Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, August 13, 2015

HUZUNI: MAMIA WAJITOKEZA KUMZIKA DEREVA BODABODA ALIYEUAWA KWA KUCHOMWA NA KISU SHINGONI.‏

Marehemu Bahati Mahela enzi za Uhai wake 
Boda Boda zimeacha Kazi na Kumsindikiza Mwenzao


 Msafara wa Boda Boda Kuelekea Makaburini 
 Gari hii ilitaka leta Mushike hapa baada ya kutaka kuchomekea
 Gari lililobeba Mwili wa Marehemu likielekea Makaburini
 Boda Boda zikiwa zimepaki Jirani na Makaburini
 Makaburini 
 Jeneza la Marehemu Mahela 
 Msemaji kwa niaba ya Familia akitoa Mwongozo 
 Maandalizi ya Mazishi
 Mazishi
 Baadhi ya waombolezaji


Picha na Mbeya yetu


MAMIA ya wakazi wa Sae jijini Mbeya wamejitokeza kwa wingi kumzika aliyekuwa mwendesha boda boda (pikipiki) aliyefahamika kwa jina la Bahati Mahela (23).
Marehemu alipatwa na mauti  wakati anapatiwa matibabu hospitali ya Rufaa jijini Mbeya baada ya kuchomwa kisu shingoni na mtu ambaye hakuufahamika ambaye alizikwa katika makaburi ya Halmashauri Mlima James Veta jijini Mbeya.
Kamanda wa Polisi alithibitisha kutokea kwa tokio hilo na kuongeza kuwa lilitokea tarehe  10.08.2015 majira ya saa mbili  usiku huko eneo la Ituha baada ya marehemu kukodishwa na abiria asiyemfahamu kutoka kijiwe cha Sae kwenda shule ya Msingi Ituha na ndipo wakiwa njiani alichomwa kisu shingoni na kisha kumpora pikipiki yake yenye namba za usajili MC 851 ABG aina ya Kinglion.
Alisema kufuatia tukio hilo msako umefanyika na pikipiki imepatikana ikiwa imetelekezwa eneo la Uyole na chanzo cha kifo chake ni kutokwa damu nyingi baada ya kuchomwa kisu shingoni na kiini cha tukio hili ni kuwania mali.
Alisema  upelelezi unaendelea ikiwa ni pamoja na kumtafuta aliyehusika katika tukio hilo.
Kwa upande wake baadhi ya viongozi wa chama cha Bodaboda (UWABOM) walilaani vikali vitendo hivyo na kuongeza kuwa Jeshi la Polisi linapaswa kusaidiana na madereva hao ili kumpata mharifu.

1 comment:

Anonymous said...

Mtu anatafuta riziki yake na kuepukana na wizi anauwawa. Lipi jema jamani. Anyway, apumzike kwa amani.