Friday, May 17, 2013

ZAIDI ya wanafunzi 500 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika Shule mbali mbali za Sekondari Wilayani Chunya Mkoani Mbeya wameshindwa kuripoti Mashuleni

Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Deodatus Kinawiro, amewataka Wazazi wa Wanafunzi hao kuhakikisha wanawapeleka watoto wao Shuleni haraka kabla ya kuchukuliwa kwa hatua za kisheria kwa mzazi atakayekaidi agizo hilo.




ZAIDI ya wanafunzi 500 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika Shule mbali mbali za Sekondari Wilayani Chunya Mkoani Mbeya wameshindwa kuripoti Mashuleni kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo kujiingiza katika biashara za uchimbaji wa Madini na Uvuvi.



Kutokana na hali hiyo Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Deodatus Kinawiro, amewataka Wazazi wa Wanafunzi hao kuhakikisha wanawapeleka watoto wao Shuleni haraka kabla ya kuchukuliwa kwa hatua za kisheria kwa mzazi atakayekaidi agizo hilo.



Kinawiro aliyasema hayo hivi karibuni wakati akizungumza na wananchi wa Kitongoji cha Majengo kata ya Sangambi Wilayani humo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Afisa elimu wa Wilaya kuhusu kukithiri kwa utoro wa wanafunzi mashuleni, Hivyo kuifanya Serikali kushindwa kufikia malengo yake ya kufuta ujinga miongoni mwa wananchi.



Alisema Wilaya ya Chunya inakabiliwa na Wimbi kubwa la wafugaji wenye tabia ya kuhamahama jambo ambalo husababisha kuwakatisha masomo wanafunzi ili hali wengine wakijikita kwenye shughuli za uchimbaji wa madini na uvuvi katika Ziwa Rukwa.



Alisema kufikia Mwishoni mwa mwezi huu mzazi yeyote ambaye hatampeleka Mwanaye Shule bila kujali kisingizio cha aina yoyote atakamatwa na kufikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya kumwachisha masomo mwanafunzi na kumpatia ajira kinyume cha Sheria.



Mkuu huyo wa Wilaya alisema Idadi ya watoto 500 ni kubwa sana hivyo hali hiyo ikiachwa itazalisha Wajinga wengi jambo ambalo litakuwa mzigo kwa taifa kutokana na wengine kuwa majambazi baada ya kukosa fedha kutokana na ajira walizojiingiza katika umri mdogo na kukwamisha juhudi za Serikali za kujenga Shule katika kila kata.


Kinawiro alisema Wilaya ya Chunya kitaaluma inafanya Vizuri katika ngazi ya Mkoa ukilinganisha na Wilaya zingine hivyo hayuko tayari kuona sifa hiyo inapotea kutokana na wazazi wachache kuzembea na kutokujua umuhimu wa kumsomesha mtoto, na kuongeza kuwa Halmashauri inaunga mkono juhudi za Serikali kwa kuimarisha ujenzi wa Mabweni ili kuhakikisha watoto wa kike hawakatizwi masomo kutokana na mimba zisizotarajiwa.


Wakati huo huo Mkuu huyo wa Wilaya aliwataka wafugaji wote waliohamia Wilayani Chunya kinyume cha Sheria kuondoka mara moja na atakae kaidi agizo hilo atakumbana na Operesheni kubwa ya kuwaondoa kwa nguvu ambapo kwa sasa wanafanya doria kwa kutumia ndege maalumu ili kuwabaini wahamiaji hao.


Alisema zoezi hilo litafanyika hivi karibuni baada ya kumalizi kuwabaini wafugaji waliovamia misitu na sehemu za hifadhi ambapo wanaharibu kutokana na kuwa na idadi kubwa ya mifugo ambayo huharibu mazingira ya Chunya kwa Ujumla.

  
Hivi karibuni kulifanyika zoezi la kuwaondoa wafugaji waliovamia msitu wa hifadhi wa kijiji cha Mbangala ambapo Jumla ya mifugo 1000 ilikutwa msituni humo na kufanyika uharibifu mkubwa lakini zoezi hilo liliingiliwa na hitilafu baada ya wafugaji hao jamii ya Wamang’ati kuwashambulia kwa mishale na mikuki maofisa pamoja na Askari wa Jeshi la Polisi waliokimbia kunusuru maisha yao.

Na E . Kamanga Chunya 

UMOJA wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM) na Umoja wa Wanawake (UWT) wa Chama hicho Mkoa wa Mbeya wametoa matamko makali kupinga kauli zilizotolewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Dk. Wilbroad Slaa pamoja na Mkewe juu ya Raisi Kikwete.

Mwenyekiti wa Uwt  Mkoa wa Mbeya Prisila Mbwaga alisema kama Wanawake wa Chama cha Mapinduzi hawako tayari kuona matusi yanayotolewa na Mke wa Dk Slaa Josephine Shumbusho juu ya Mama Salma Kikwete kwamba anachangia kuibomoa Nchi.
 Mwenyekiti wa Uvccm Mkoa wa Mbeya Amani Kajuna alisema Umoja wa Vijana hauko tayari kufumbia macho matusi anayotukanwa Raisi Kikwete  na Dk Slaa anapokuwa akihutubia wanachama wake jukwaani.




 
UMOJA wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM) na Umoja wa Wanawake (UWT) wa Chama hicho Mkoa wa Mbeya wametoa matamko makali kupinga kauli zilizotolewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Dk. Wilbroad Slaa pamoja na Mkewe juu ya Raisi Kikwete.


Matamko hayo yalitolewa  na Wenyeviti hao katika Mkutano na Vyombo vya habari uliofanyika katika Ofisi za UVCCM Mkoa wa Mbeya, ambapo walisema kamwe hawawezi kufumbia macho maneno ya uzushi na uchonganishi kati ya Serikali na wananchi.
  
Akisoma tamko Mwenyekiti wa Uvccm Mkoa wa Mbeya Amani Kajuna alisema Umoja wa Vijana hauko tayari kufumbia macho matusi anayotukanwa Raisi Kikwete  na Dk Slaa anapokuwa akihutubia wanachama wake jukwaani.

Alisema katika Mkutano alioufanya Mei 12, Mwaka huu Wilayani Mbozi Mkoa wa Mbeya Dk. Slaa akihutubia wananchi kuwa Raisi Kikwete ni Freemason,  Mdini, Mawaziri hawamsaidii pia ni Mafisadi na kuongeza kuwa ana ushahidi wa  Cd ambazo Raisi Kikwete akihamasisha udini na kuhusu uchinjaji.

Alisema maneno ya Dk. Slaa ni uzushi ambao unalengo la kufitinisha Watanzania na Serikali ya Chama cha Mapinduzi hususani anapofanya mikutano ya Hadhara katika Mkoa wa Mbeya ambapo aliongeza kuwa Ufisadi anaousema yeye kwa Mawaziri wa Ccm ili hali yeye mwenyewe anaongoza kwa ubadhilifu wa fedha za Wananchi.

Alitolea mfano wa ubadhilifu uliofanywa na Chadema mkoani Mbeya kuwa ni pamoja na Kitendo chaMwenyekiti wao Freemani Mbowe kuchangisha fedha Milioni Tatu kwa wananchi kwa kile alichodai zingetumika kununulia maji na matibabu wakati wa maandamano lakini hazikufanya kazi hiyo na hazijulikani zilipo.


Kajuna alisema mbali na fedha hizo kutokujulikana matumizi yake  pia Dk. Slaa alichangisha fedha zingine Shilingi Laki saba kwa ajili ya posho ya Wabunge waliofukuzwa bungeni jambo ambalo lilileta sintofahamu kwa wakazi wa Jiji la Mbeya.


Alisema ufisadi mkubwa uliopo ndani ya Chadema ambao kila Mwezi wanapata ruzuku ya takribani Milion mia Tatu lakini hawajawahi kujenga hata chumba kimoja cha Zahanati wala kutoa msaada kwa wananchi wasiojiweza lakini wao wanazidi kuwachangisha wananchi.


“ Jamani watanzania fungukeni muone huyu kiongozi wa namna gani Mlafi, Mchoyo na mchochezi  asiyependa kuona amani ya Nchi ikistawi” alisema Kajuna.


Aliongeza kuwa pamoja na Chadema kupata fedha zote hizo bado zinaishia mikononi mwa watu wachache hususani Dar Es Salaam ambapo Mikoani hawazipati na ndiyo sababu Ofisi za Chadema Mkoa wa Mbeya zilifungwa kutokana na kutolipia pango la Nyumba deni la Shilingi Laki tatu.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Uwt Prisila Mbwaga alisema kama Wanawake wa Chama cha Mapinduzi hawako tayari kuona matusi yanayotolewa na Mke wa Dk Slaa Josephine Shumbusho juu ya Mama Salma Kikwete kwamba anachangia kuibomoa Nchi.


Alisema Shumbusho alinukuliwa akitoa matusi makubwa dhidi ya Mama Salma katika mkutano wa hadhara uliofanyika Wilayani Mbozi akisema ameshindwa kumshauri raisi kuhusu uongozi na namna ya kuongoza nchi.

Aliongeza kuwa katika matusi yake alimtuhumu Mke wa Raisi kuwa ni Mwanamke Mpumbavu anayeibomoa nchi nyumba yake kwa mikono yake Mwenyewe kama Biblia inavyosema na kwamba yeye atakuwa tayari kumshauri Dk. Slaa atakapokuwa Raisi mwaka 2015.


Kutokana na tuhuma hizo Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Mbeya wamemtaka Mke wa Dk. Slaa kuacha tabia ya kumsema vibaya Mama Salma na akiendelea hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Picha na Mbeya yetu

Tuesday, May 14, 2013

AJALI TENA WILAYANI RUGWE MKOANI MBEYA JIONI YA LEO MMOJA AHOFIWA KUFA MAJERUHI MWINGINE APELEKWA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA

AJALI MBAYA IMETOKEA LEO JIONI MAENEO YA KANYEGELE KIWIRA WILAYANI RUNGWE ENEO HILO MAALUFU KWA JINA LA UWANJA WA NDEGE LORI LILILOKUWA NA SHEHENA YA CHUPA LIKITOKEA DSM KUELEKEA NCHINI MALAWI LILIKATIKA BLEKI NA KUPAA KUINGIA MSITU NDANI YA LORI HILO KULIKUWA NA DEREVA PAMOJA NA TINGO WAKE MASHUHUDA WA AJALI HIYO WAMESEMA HUWENDA MMOJA AMEFARIKI ILA MWINGINE HALI YAKE INASEMEKANA NI MBAYA 


MKUU WA WILAYA RUNGE AKISIMULIWA NA MOJA WA MASHUHUDA WA AJALI HIYO







PICHA KWA HISANI YA RICHARD  MCHINA    RUNGWE

Habari ya tukio zima tutawaletea kesho baada ya kupata taarifa iliyokamilika

AJALI MBAYA IMETOKEA MCHANA WA LEO WATATU WAFARIKI PAPO HAPO BAADA YA ROLI KUPINDUKA BARABARA YA CHUNYA MAENEO YA MWANSEKWA

JINAMIZI  LA AJALI LINAZIDI KUIKUMBA MBEYA WATU WATATU  WAMEFARIKI PAPO HAPO BAADA YA ROLI LA KAMPUNI YA KICHINA LILILOKUWA LIMEBEBA KIFUSI KUKATIKA BREKI NA KUPINDUKA MAENEO YA MWANSEKWA BARABARA YA CHUNYA MCHANA WA SAA 7 MPAKA SASA MAITI MBILI ZIMETAMBULIWA NA MOJA IMEHARIBIKA VIBAYA SANA KIASI CHA KUSHINDWA KUTAMBULIWA 
BAADHI YA WACHINA WANAOTENGENEZA BARABARA YA CHUNYA WAKIWASIKILIZA WANANCHI WALIOSHUHUDIA AJALI HIYO IKITOKEA
BAADHI YA MAJERUHI WAKISUBIRI KUPATA HUDUMA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA  MPAKA TUNA TOKA HOSPITALINI HAPO TUMEACHA MAJERUHI WATANO WAKIENDELEA KUPATA MATIBABU


Picha na Mbeya yetu

Monday, May 13, 2013

AJALI MBAYA IMETOKEA MBALIZI MBEYA MMOJA AFARIKI PAPO HAPO NA WANNE MAJERUHI


MAREHEMU SELEMANI JUMA SELEMANI ALIYEKUWA TINGO WA ROLI HILO AMEFARIKI PAPO HAPO 


AJALI HII IMETOKEA KWENYE MTEREMKO WA MBALIZI ROLI HILO INA SEMKANA LILI FERI BREKI









HABARI KAMILI YA AJALI HII TUTAWALETEA BAADAE

AJALI YAUA MMOJA NA MAJERUHI 17 WALAZWA WILAYANI RUNGWE

GARI YA AINA YA COSTA T 399 AUD ILIYOGONGWA KWA NYUMA NA KISHA KUPINDUKA ENEO LA KANYEGELE UWANJA WA NDEGE WILAYANI RUNGWE

HUU NI UPANDE WA NYUMA WA COSTA HIYO 


BAADHI YA WASIO WASAMARIA WEMA WAKITAFUTA FEDHA ZILIZODONDOKA KUTOKA KATIKA BASI HILO HATA HIVYO VIJANA HAO WALIZOMEWA NA WANANCHI WALIOFIKA KUTOA MSAADA


HILI NDILO ROLI LILILO IGONGA COSTA KWA NYUMBA NA KUSABABISHA AJALI HIYO NAMBARI YA ROLI T 712 CZC NA TERA LENYE NAMBALI T 444 CCZ LIKIWA NA SHEHENA YA MBOLEA


MOJA KATI YA MAJERUHI AKIWA KATIKA HOSPITALI YA TUKUYU

BAADHI YA MAJERUHI WAKISUBIRI HUDUMA


BAADHI YA NDUGU WAKISUBIRIA KUWAONA NDUGU ZAO WALIOPATA AJALI

BAADHI YA WAGONJWA WAKISAFIRISHWA KWENDA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA



KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA RUNGWE ILIPOTEMBELEA MAJERUHI WALIOPATA AJALI




                                                                               

                     Picha na  Ezekiel Kamanga