Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, August 12, 2015

TAASISI YA KILAWA ENTERPRISES YAJIKITA KUTOA ELIMU KWA WAKULIMA

 Afisa Masoko wa Kilawa Enterprises, Award Mpandila akitoa maelekezo kwa wakulima waliotembelea banda lao.

 Afisa Masoko wa Kilawa Enterprises, Award Mpandila akigawa vipeperushi kwa wakulima waliotembelea banda lao.

Mkulima Japhet Kihupi akitoa maelezo kwa wakulima wenzake waliofika kutembelea shamba darasa linalosimamiwa na Kilawa Enterprises.

Mkurugenzi wa Kilawa Enterprises, Tito Tweve akifuatilia kwa makini mafunzo ya wakulima katika shamba darasa.

Mtaalam wa kilimo cha Mpunga, Sabiti Njovu akitoa maelekezo kwa wakulima juu ya upandaji wa mpunga.

Wakulima wakiangalia mashine zinazotumika kupandikizia mpunga walipofika kujifunza katika maonesho ya nanenane.
 

 
KATIKA kuhakikisha Wakulima wanaondokana na kilimo cha mazoea, Taasisi ya Kilawa Enterprises ya mkoani Mbeya imejikita katika utoaji wa elimu juu ya matumizi sahihi ya pembejeo za kisasa kwa kilimo bora.
 
Wito huo ulitolewa na Meneja Masoko wa Taasisi hiyo, Award Mpandila alipokuwa akitoa elimu kwa wakulima waliotembelea banda lao katika maonesho ya wakulima nanenane yaliyomalizika hivi karibuni ambapo alisema lengo la Taasisi hiyo ni kumsaidia mkulima wa hali ya chini aweze kuongeza uzalishaji kwa kufuata kanuni bora za kilimo.
 
Alisema wakulima hufundishwa mambo mbali mbali yakiwemo namna ya kuandaa shamba mapema kabla ya mvua za kwanza kunyesha kuanziua mwezi Septemba na Oktoba na kasha kupanda baada ya mvua kunyesha mwezi Oktoba na Novemba.
 
Alisema elimu nyingine wanayompatia mkulima ni pamoja na kupanda kwa kutumia mvua za kwanza, matumizi ya mbegu bora, upandaji wa nafasi kwa kutumia vipimo sahihi na matumizi ya mbolea ili kupata mavuno mengi.
 
Mpandila alisema wakulima hao wakipata elimu hiyo sambamba na kukumbushwa palizi kwa ajili ya kuondoa magugu mashambani kulingana na aina ya mazao pamoja na kuzuia wadudu waharibifu pamoja na magonjwa mbali mbali yanayoharibu mazao.
 
Aliongeza kuwa pamoja na elimu hiyo bado wakulima wanatatizo la kutowahi kuvuna mazao yao mara baada ya kukomaa jambo linalopelekea upotevu wa mazao mashambani ambapo pia hufundishwa namna ya kuhifadjhi ghalani na kuanza kusafisha shamba kabla ya msimu wa kilimo kuanza.
 
Mwisho.
 
                                                                                                                         

No comments: