Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Saturday, June 27, 2015

NYALANDU AWASHUKURU WANACHAMA WA CCM WALIOJITOKEZA KUMDHAMINI MBEYA

WAZIRI wa Maliasili na utalii,Lazaro Nyalandu akiongea na waandishi wa habari wa mkoa Mbeya





 

WAZIRI wa Maliasili na utalii,Lazaro Nyalandu amewashukuru wanachama wa CCM Mkoa wa Mbeya waliojitokeza kumdhamini katika harakati za kuwania kuteuliwa kugombea urais.

Licha ya kuwashukuru wanachama hao lakini Waziri Nyalandu aligoma kutaja idadi ya wadhamini aliowapata na kudai kuwa atakachokiwasilisha makao makuu ya Chama ni Idadi ya wadhamini inayotakiwa.


Nyalandu aliyasema hayo  alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ziara yake ya kutafuta wadhamini kutoka kwa wanachama wa Chama cha Mapinduzi ili aweze kuteuliwa kuipeperusha bendera katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu ujao.


Alisema ndani ya CCM kuna Demokrasia kubwa hali iliyopelekea wanachama kujitokeza kwa wingi kutaka kugombea Urais lakini kikubwa ni kila mgombea kuweka maslahi ya Chama mbele ili kuimarisha umoja na mshikamano na kuwavutia walio nje ya Chama kujiunga nacho.


Aliongeza kuwa katika mchakato huo mwisho wa siku Chama kitamteua mtu mmoja atakayesimama na kupeperusha bendera katika uchaguzi huo hivyo wagombea wote watapaswa kumuunga mkono ili Chama kiweze kuibuka na usgindi mkubwa na kishindo.


 Waziri Nyalandu alisema katika kinyang’anyiro hicho amejifunza mambo mengi ambayo yamemsukuma na yeye kuingia humo likiwemo kupanuka kwa demokrasia ndani ya Chama na jinsi wanachama wengi walivyojitokeza kuichukua fomu za kuteuliwa kugombea Urais.


 Alisema jambo lingine ni changamoto zinazowakabili wananchi wa kawaida pamoja na jinsi Nchi ilivyopiga hatua katika maeneo mbali mbali chini ya uongozi wa Rais wa awamu ya nne na kuongeza kuwa Rais ajaye hatakuwa na budi ya kufuata nyendo zake katika uongozi wake.


Alisema kama akiteuliwa na kushinda Urais atahakikisha anawekeza katika rasilimali watu katika kuwawezesha kukabiliana na changamoto zinazojitokeza za wakati kwa kutumia fursa zilizopo pamoja na kuwezesha vijana ili waweze kulitumikia Taifa.


Kuhusu idadi ya Wadhamini aliowapata katika ,ikoa yote aliyopita Nyalandu alisema amebakiza mikoa mitatu ambayo lazima akamilishe lakini idadi ya wadhamini amesema atawasilisha idadi inayotakiwa na Chama ya wadhamini 450  tu na sio vinginevyo.



Mwisho.

No comments: