Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, June 30, 2015

Wagombea 26 kati 39 warejesha fomu Mbozi Mashariki

Mtiania nafasi ya Ubunge jimbo la Mbozi Magharibi,Abraham Msyete.akizungumza na wananchi wa mji wa Vwawa,  katika ofisi za chama Wilaya mara baada ya ya kurejesha fomun ya kuomba ridhaa ya kuwania nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadsema) kushoto ni mama yake mzazi Luendeni Msyete (Picha na Kenneth Ngelesi)




JUMLA ya watiania 26 kutoka jimbo la Mbozi Mashariki wamerejesha fomu katika ofisi za Wilaya, kati 39 ambao walijitokeza kuomba ridhaa ya kupeperusha bendera cha chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa nafasi ya Ubunge katika uchaguzi Mkuu mwaka huu.




 Baada ya kurejesha fomu hizo baadhi ya wagombea walijinasibu kuwa wanauwezo wa kutumikia jamii katika nafasi ya Ubunge endepo chama  kitawapa ridhaaa ya kupeperesha bendera kutoka na uwezo wao wa kujenga hoja na kulifahamu jimbo hilo vizuri kutoka kuwa wazawa lakini pia wamekukitumikia chama hicho kwa muda mrefu.




Abaraham Msyete ambaye ni mmoja wawatiania alisema kutokana na kukitumia chama hicho kwa zaidi ya miaka kumi,huku akifanya kazi mbalimbali za kukimarisha chama hivyo ameamua kuchukua fomu na kuomba chama kiwezi kumpitisha kwani amejitafakari na kuona anaweza kuwatumia wananchi wa Jimbo la Mbozi Mashariki na taifa kwa ujumla katika nafasi ya Ubunge.




‘Nina ozeofu na jimbo hili na kwani nimezaliwa Mbozi na kusoma Mbozi hivyo na pia nimeanza harakati za kukinadi chama tangu nikiwa mwanafunzi wa Chuo kikuu cha Dar-es-laamu, hivyo mpaka sasa ni zaidi ya kumi nipo ndani ya Chadema ni imania yangu chama kitanipa ridhaa ya kupeperusha bendera katika uchagu ujao’alisema Msyete
Mbali na hilo lakini  Msyete alibainisha baadhi ya Mambo kumi ambayo anayapa kipaumbele ambavyo atapaswa kuyatekekeleza mara tu atakuwa Mbunge wa jimbo hilo.




Msyete alisema kuwa baadhi yake  ni uboreshaji wa kilimo chenye tija,miondombinu ya barabara,maji,ajira kwa vijana,elimu,wa huduma afya pamoja na kupiginia haki kwa wakulima.




Katika sekta ya elimu Msyete alisema kuwa Wilaya Mbozi yenye wakazi zaidi ya 490,000/ na shule nyingi za msingi na Sekondari lakini hakuna chuo cha ufundi hata kimoja ambacho kingeweza kuwaanda vijana kuwa mafundi ambayo ni fursa pekee kwao kuweza kuji ajiri.




Kwa upande wake Stephen Mwamengo alisema Mbozi,inakabiliwa na na matatizo mengi tangu kupata Uhuru na hilo ndiyo yaliyo msukumwa kuchukua fomu na kuomba ridhaa kupitia chama chake kiwezo kupitisjha ili awe mgombea Ubunge.




Alisema kuwa jimbo la Mbozi Mashariki limejaliwa rasilimali nyingi ikiwemo ardhi yenye rutuba lakini viongozi waliotangulia katika awamu zote hawajaweza kuwasadia wananchi kuondokana na umasimni kutoka na ardhi hiyo.

Alisema kuwa endapo atachaguliwa hatau ya kwaza ni kuwapigia wananchi wawezi kutambua umuhimu wa ardhi wanayo miliki na ili kuweza kapata hata mikopo katika taasisi za fedha ili kupata mikopo.




Hata hivyo katika jimbo hilo la Mbozi Mashariki kumekuwa na sitofahamu kutoka na watia nia hao kuchukua na kurejesha fumu zao katika ofisi mbili tofauti huku kila upande ukidai kuwa unahaki ya kulisimamia zoezi huku kiloa upande ukisema kuwa Ofisi zao ni za Wilaya.




Katika ofisi ya kwanza ambayo msimamizi wa zoezi la kuchukua na urejeshaji wa fomu ni Michael Mwamlima ambaye ni katibu wa Bavicha, amabaye aliieleza Tanzania Daima kuwa kuwa katika ofisi hiyo watia nia walikuwa nane na wote walichukua fomu na wato nane ndiyo walio zirejesha.




Aidha katika ofisi nyingine ambayo msimamizi wa zoezi hilo,Osward Mweluka ambaye alijinasibu kuwa ni kaimu Katibu wa chama hicho ngazi ya Wilaya ya Mbozi alisema katika ofisi hiyo watia nia walikuwa 29 walio chukua fomu ni 18 na ndiyo walio rejesha.











No comments: