Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, May 7, 2015

WAZEE WA BARAZA WAINGILIA KATI MGOGORO WA KANISA LA MORAVIANI MBEYA.




 Mwenyekiti wa baraza la wazee wa Moravian Jimbo la Kusini Magharibi, Frank Phiri akitoa tamko kwa waandishi wa habari.
 Mwenyekiti wa baraza la wazee wa Moravian Jimbo la Kusini Magharibi, Frank Phiri akiwa na waandishi wa habari.
 Waandishi wa Habari wakimsikiliza Mwenyekiti wa baraza la wazee.
WAJUMBE wa Baraza la wazee wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Magharibi wameingilia kati mgogoro uliodumu ndani ya kanisa hilo kwa muda wa miaka miwili.
 
Mgogoro huo uliodumu kwa miaka miwili umekuwa ukiwahusisha Askofu wa Jimbo hilo, Alinikisa Cheyo na Mwenyekiti wa Jimbo Mchungaji Nosigwe Buya  pamoja na Halmashauri kuu ya kanisa.
 
Kutokana na kudumu kwa mgogoro huo ndani ya kanisa, Baraza la wazee wa Moravian Jimbo la kusini magharibi limetoa tamko la kumlaani Askofu Alinikisa Cheyo na Halmashauri kuu kwa kushindwa kutatua na kumaliza mgogoro huo.
 
Akisoma tamko hilo kwa vyombo vya habari, Mwenyekiti wa Mabaraza ya Wazee, Frank Phiri, alisema kwa kipindi hicho cha miaka miwiliimeonekana Wajumbe wa Halmashauri kuu na Askofu Alinikisa Cheyo wanauendeleza mgogoro huo na hawataki maridhiano ndani ya kanisa.
 
Phiri alisema kitendo hicho kinalitia aibu Kanisa ambapo wakristo kupitia mabaraza ya wazee kutoka shirika mbali mbali za jimbo la Kusini magharibi hawakuchoka kutafuta amani ndani ya kanisa ambapo walikutana Mei 2, mwaka huu na kupitia mwenendo wa mgogoro huo.
 
Alisema baada ya kupitia mwenendo mzima baraza hilo liliazimia na kukubaliana kumtambua Mchungaji Nosigwe Buya kama Mwenyekiti halali wa Kanisa la Moravian Jimbo la kusini magharibi tangu alivyochaguliwa Oktoba 2012.
 
Alisema makubaliano mengine Baraza linamuagiza Mwenyekiti Buya kuitisha Sinodi ya pekee haraka iwezekanavyo, wajumbe wa Halmashauri kuu wanatakiwa kusimamia Katiba ya Moravian na kutopeleka masuala ya kanisa mahakamani.
 
Aliongeza kuwa Baraza la wazee pia linawatambua Wachungaji wote waliosimamishwa kutoa huduma kutokana na mgogoro huo na kuwataka kuendelea na kazi yao ya kuhubiri.
 
Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa kutokana na ukiukaji wa maksudi na wazi wazi wa katiba ya kanisa la Moravian Tanzania, Baraza limeiagiza Halmasahuri kuu ya Jimbo kutomzuia kwa namna yoyote kufanya kazi kama Mwenyekiti Mchungaji Nosigwe Buya.
 
“ Kwa kuwa Mwenyekiti ameagizwa kumaliza mgogoro kwa njia ya sinodi, hatutegemei tena kusikia malumbano au kumzuia kufanya kazi ya Mungu kama tulivyo watuma na bwana alivyowaweka katika shamba lake, tunaomba wachungaji na wakristo tuendelee kuiombea Sinodi iliyo mbele yetu ili kuleta amani, upendo, umoja na mshikamano wa kanisa kama Mwanzo” alisisitiza Mchungaji huyo.
 
Na Mbeya yetu

    No comments: