Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, May 13, 2015

MWIGULU ACHANGISHA MILIONI 53 KWENYE HARAMBEE YA KANISA‏

 Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba akitoa hutuba katika harambee ya kanisa la GMCL
 Mchungaji Aquina Mhanze akisoma risala ya kanisa mbele ya mgeni rasmi
 Nabii Mpanji akihubiri kabla ya kuanza kwa harambee
 Naibu Waziri pamoja na meza kuu wakicheza moja ya nyimbo zilizoimbwa kanisani hapo.
 
Waumini wakifuatilia Ibada ya Harambee kanisani hapo
                                                                                                      
    NAIBU Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba(Mb) jana aliwaongoza mamia ya waumini Kanisa la GMCL lililopo Ilomba jijini Mbeya kukusanya fedha  zaidi ya shilingi Milioni 53 katika harambee ya kuchangia miradi ya Kanisa hilo.

    Katika Harambee hiyo ambayo Mwigulu Nchemba alikuwa mgeni rasmi zilipatikana fedha taslimu shilingi Milioni 2.7 na Ahadi shilingi Milion 50,235,000 na  kufanya jumla kufikia shilingi Milioni 53,017000.

    Awali wakisoma risala ya Kanisa mbele ya mgeni rasmi iliyosomwa na Mchungaji Aquina Mhanze, walisema Kanisa limekuwa likiendesha ibada zake kwa njia ya vyombo vya habari ili kuwafikia waumini wengi jambo ambalo linagharimu fedha nyingi za kuendeshea zoezi hilo.

    Mchungaji Mhanze alisema huduma hiyo ilianza mwaka 2012 ambapo zaidi ya shilingi Milioni 40 zilikuwa zikitumika fedha ambazo zilikuwa ni michango ya waumini ambazo kila muumini alilazimika kuchanga shilingi 5000 hadi 10,000 kwa mwezi ili kufanikisha huduma hiyo.

    Alisema baada ya kuona zoezi hilo linakuwa gumu wakaunda kamati maalumu ambayo ilipewa jukumu la kuhakikisha wanakuwa na kituo cha Redio, ambapo zilihitajika Shilingi Bilioni Moja kuanzisha redio hiyo lakini fedha zilizopatikana hadi Mwaka jana zilikua Shilingi Milioni 150 ambazo zilifanikisha kuanzisha kituo cha Redio cha GMCL fm.

    Alisema pamoja na kufanikiwa kuanzisha redio hiyo bado inakabiliwa na changamoto ambazo zimelazimu kuitishwa kwa harambee hiyo ambazo kukosekana kwa ubora wa matangazo yanayotokana na ukosefu wa Standby Jenereta ili kukabiliana na umeme unapokatika, vyuma vya kurefushia mnara na Transmita vitu vinavyogharimu Shilingi Milioni 50.

    Alisema Changamoto nyingine ni ukosefu wa ofisi kwa ajili ya kuendeshea redio hiyo inayogharimu shilingi Milioni 150 hivyo kufanya jumla ya shilingi Milioni 200 kuhitajika kwa ajili ya kukamilishia miradi ya Kanisa hilo.

    akijibu Risala hiyo Mwigulu Nchemba alilipongeza Kanisa kwa juhudi za kuongeza miradi kuwa jambo hilo linaelekea kuwakomboa Watanzania na kuwajenga katika imani ili wawe na hofu ya kumjua Mungu.

    Alisema mbali na kuwaongoza waumini kuchangisha shilingi Milioni 53,017,000 pia atakuwa Miongoni mwa Wanakamati ili kuhakikisha malengo ya kukamilisha miradi hiyo inafanikiwa ikiwa ni pamoja na kuwaunganisha na marafiki zake wanaoishi nje ya Mkoa wa Mbeya.

    “Niongezeni kwenye kamati yenu lengo sio kumaliza na kukamilisha ratiba ya leo bali ni kutimiza  yaliyokusudiwa, mmelenga kuniita mimi kwani kila mnachoongelea ni Injili, Kanisa na Miradi hilo lina baraka sana na laiti Watanzania wangejua umuhimu wa injili haya yanayolikumba Taifa yasingetokea” Alisem Naibu Waziri.

    Na Mbeya yetu





       

    No comments: