Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Monday, May 18, 2015

MABATINI KINARA REDCROOS CUP 2015‏

 Mwenyekiti wa Redcross Mkoa wa Mbeya, Ulimboka Mwakilili akizungumza na timu muda mfupi kabla hazijaingia uwanjani.
 Timu zikisalimiana.
Wachezaji wa Timu ya Ghana wakiwa katika picha ya pamoja
 Wachezaji wa Timu ya Mabatini wakiwa katika picha ya pamoja
 Timu zikiwa uwanjani zikitimua vumbi.
Wachezaji wa timu ya mabatini wakishangilia baada ya kuibuka mabingwa

TIMU ya Kombaini ya Kata ya Mabatini ilifanikiwa kuibuka kidedea katika fainali za Kombe la Red Cross 2015 zilizofanyika Mei 8, mwaka huu katika viwanja vya shule ya Msingi RuanzaNzovwe baada ya kuifunga Goli Moja kwa bila timu ya Kombaini ya Kata ya Ghana.
 
Mchezaji Daniel William aliiwezesha timu yake ya Mabatini kupata goli la ushindi dakika ya 30 ya kipindi cha kwanza cha mchezo baada ya kuwazidi ujanja walinzi wa timu ya Ghana.
 
Kutokana na ushindi huo Timu ya Mabatini ilijinyakulia Kikombe, Jezi seti moja 15 na Mpira mmoja huku timu ya Ghana ambao ni mshindi wa Pili akijinyakulia Seti moja ya Jezi 15 na Mpira mmoja na Mshindi wa tatu ilikuwa Kata ya Ilomba walioambulia Jezi Seti moja.
 
Akizungumza wakati wa kufunga mashindano hayo, Mwenyekiti wa Chama cha Msalaba Mwekundu(Redcross)Mkoa wa Mbeya, Ulimboka Mwakilili alisema ligi hiyo hufanyika kila mwaka ikiwa ni maadhimisho ya msalaba mwekundu duniani.
 
Alisema Ligi iyo ilianza kutimia vumbi Aprili 27, Mwaka huu kwa kuzikutanisha timu kutoka katika Kata 12 ambazo ni Mabatini, Nzovwe, Iyela,Ghana, Isyesye, Ruanda, Ilemi, Uyole, Mwakibete, Iyunga, Ilomba na Isanga.
 
Alisema lengo la michuano hiyo ni kutoa burudani kwa wakazi wa Jiji la Mbeya pamoja na kuinua vipaji ambapo katika mashindano hayo watachaguliwa vijana 25 watakaounda timu ya Mkoa itakayofanya ziara katika mikoa ya Arusha na Morogoro.
 
Aliongeza kuwa mbali na ziara hiyo pia watachambuliwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 ambao wataweza kutembelea Nchi za Nje ambazo ni wanachama wa Redcross kwa kucheza nazo michozo kadhaa.
 
Na Mbeya Yetu    

No comments: