Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, September 12, 2014

TUNAWATAMBULISHA KWENU MSANII MKALI WA MIONDOKO YA BONGO FLEVA KUTOKA JIJINI MBEYA SHUKRANI JAITO A.K.A SJ

 Msanii wa Muziki wa kizazi Kipya Bongo Fleva Shukrani Jaito(SJ) wa kwanza kushoto akiendelea na Mahojiano na Mwandishi wa Habari Venance Matinya
Mwandishi wa Habari Venance Matinya wa kwanza Kulia akichukua maelezo kutoka kwa Msanii wa Bongo Fleva Shukrani Jaito(SJ)



WADAU wa mziki wa kizazi kipya maarufu kwa Bongofleva wametakiwa kuwapa nguvu wasanii wanaochipukia ili kuwawezesha kufikia malengo na mafanikio  katika Tasnia ya kutoa elimu na burudani kupitia sanaa hiyo.

Wito huo umetolewa na msaanii anayeibukia wa Jijini Mbeya, Shukrani Jaito(SJ) alipokuwa akizungumzia changamoto anazokumbana nazo katika kusakla riziki kwenye tasnia ya Muziki wa kizazi kipya katika Mahojiano maalumu na Mtandao Mbeya yetu Blog

Shukrani alisema changamoto kubwa anayokabiliana nayo na ambayo anaomba msaada kutoka kwa wasamaria wema ni kumuwezesha kufika katika studio kubwa ili aweze kurekodi nyimbo zake na hatimaye kupigwa kwenye vyombo mbali mbali vya habari hapa nchini.

Alisema pia anahitaji msaada wa kupata mdhamni ambaye atakuwa msimamizi wa kazi zake, kumuandalia matamasha pamoja na kumpa ushauri juu ya namna mbali mbali za kufanya ili aweze kuinua kipaji chake hicho cha mzuki wa kizazi kipya.

Aidha ametoa shukrani kwa Jacob Mwaisango aliyemsaidia kwa kiasi Fulani hadi ameweza kurekodi nyimbo tatu pamoja na kumpa fedha kwa ajili ya matumizi madogo madogo ingawa peke yake hatoweza hivyo anatoa wito kwa wadau wengine kuiga mfano huo.

Akizungumzia historia yake anaseme alianza kuwa na kipaji cha kuimba tangu akiwa shule ya msingi darasa la Tano hali iliyowapelekea baadhi ya walimu kumbatiza jina la msanii lakini hakuweza kurekodi nyimbo yoyote.

Alisema hivi sasa ana nyimbo tatu ambazo alianza kurekodi wimbo wa kwanza mwaka 2012 unaoitwa Pesa chini ya studio ya Moja moja recird iliyoko Ilemi, Wimbo wa Pili uliorekodiwa mwaka huu unaoitwa Bila wewe pamoja na Mama alizorekodi H studio iliyopo Isanga jijini Mbeya.


Alisema hivi sasa anajipanga kurekodi wimbo mmoja na msanii mkubwa ambaye ndiye ndoto yake na anayefuata nyayo zake, Ali Kiba hivyo anaomba wadau kumsaidia kwa hali na mali ili aweze kukutanishwa na msanii huyo pamoja na fedha za kuingilia studio.

Na Mbeya yetu

No comments: