Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Saturday, May 3, 2014

Timu ya Taifa ya Malawi imefurahishwa na mapokezi mazuri waliyoyapata Mkoani Mbeya na kuahidi kuonesha kandanda safi kati yake na timu ya Taifa(Taifa stars).


 Kiongozi wa msafara wa Timu ya Malawi Mrs Flora Mwandira akiongea na waandishi wa habari wa mkoa wa Mbeya

Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mbeya(MREFA)Seleman Harubu amewataka washabiki kufika kwa uwingi uwanjani na kuishangilia timu yao ya Taifa kwa amani na utulivu ili kuenzi heshima iliyopewa Mkoa wa Mbeya kwa TFF kukubali mchezo huo kufanyika Mkoani hapa.

Mwalimu wa timu hiyo Young Chimodzi 


Add caption


Timu ya Taifa ya Malawi imefurahishwa na mapokezi mazuri waliyoyapata Mkoani Mbeya na kuahidi kuonesha kandanda safi kati yake na timu ya Taifa(Taifa stars).

Kauli hiyo imetolewa na Kiongozi wa msafara huo Mrs Flora Mwandira na kuungwa mkono na Mwalimu mkuu wa timu hiyo Young Chimodzi aliyewahi kuichezea timu ya Taifa ya Malawi kwa miaka kadhaa.

Mwandira amesema Timu ya Malawi imewasili na msafara wa wachezaji 20 na viongozi 12 ambao waliwasili siku ya alhamisi jioni na kufanya mazoezi katika uwanja wa Sokoine.

Mchezo huo umevuta hisia za watu wengi umevuta hisia za wakazi wa Jiji la Mbeya na Mikoa ya Jirani na kufanya nyumba nyingi za wageni kujaa.

Mwalimu wa timu hiyo ameweka hadharani wachezaji waliwasili kupambana na Taifa Stars kuwa ni Makipa Charles Swin na Richard Chipuwa na Walinzi Pirilani Zonda,Francis Mulimbika,John Lanjesi,Emmanuel Zoya,Bashiri Maunde na George Nyirenda.

Wachezaji wa kiungo ni pamoja na John Banda,Mecium Mhone,Douglas Chirambo,World Nkuliwa,Frank Banda,Junior Chimodzi,Phillip Masiye na Ndaziona Chatsalira.

Washambuliaji ni Gaston Simukonda,Green Harawa,Diverson Mlozi na Rodrick Gonani.

Kwa upande wa chama cha mpira nchini kimetangaza kuwa kiingilio katika mchezo huo kitakuwa ni shilingi 5000 na hakuna magari yatakayo ruhusiwa kuingia uwanjani isipokuwa magari ya wachezaji,Polisi na Gari la wagonjwa na tiketi zitaanza kuuzwa saa mbili asubuhi siku ya Jumapili katika vituo mbali mbali Jijini Mbeya.

Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mbeya(MREFA)Seleman Harubu amewataka washabiki kufika kwa uwingi uwanjani na kuishangilia timu yao ya Taifa kwa amani na utulivu ili kuenzi heshima iliyopewa Mkoa wa Mbeya kwa TFF kukubali mchezo huo kufanyika Mkoani hapa.

Mbeya yetu

No comments: