Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, May 6, 2014

SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA KUNAWA MIKONO ZAFANA MBEYA

Baadhi ya wananchi na wafanyakazi wa wa hospitali ya Rufaa Mbeya wakiandamana na mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya kunawa mikono Duniani




Moja ya wauguzi akionyesha mfano wa kunawa mikono Mbele ya mgeni rasmi

Mama moja  kati ya wananchi waliohudhuria sherehe hizo akinawa mikono kuonyesha anajili afya yake

Risara ikisomwa mbele ya mgeni rasmi

Burudani mbalimbali zilikuwepo katika sherehe hiyo

Ngonjera inaendelea


Moja ya manesi Rose Ndagala akitumbuiza siku hio huku wenzake wakimuunga mkono kucheza


 Mgeni Rasmi Adrian Majembe amesema kuwa jukumu la kunawa mikono lisiishie kwa wageni wanaoingia na kutoka Hospitali bali pia wauguzi nao wanalo jukumu la kunawa  kabla na baada pindi wanapowahudumia wagonjwa Hospitalini.

Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa Daktari Humprey Kihwelo alieleza umuhimu wa kunawa mikono kwa usahihi ikiwa ni juhudi za kuzuia magonjwa ya maambukizi kama vile kuhara na magonjwa ya ngozi.





Picha ya pamoja



Sherehe za Maadhimisho ya kunawa mikono Duniani yameadhimishwa Mei tano mwaka huu katika maeneo mbalimbali na Mkoani Mbeya yameadhimishwa  katika Hospitali ya Rufaa na Mgeni rasmi alikuwa Adrian Majembe.

Awali Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa Daktari Humprey Kihwelo alieleza umuhimu wa kunawa mikono kwa usahihi ikiwa ni juhudi za kuzuia magonjwa ya maambukizi kama vile kuhara na magonjwa ya ngozi.

Kihwelo amewataka wananchi wanaoingia  na kutoka katika Hospitali kunawa,pia wanapofamya shughuli mbalimbali wanawe mikono ili kuepuka magonjwa ya maambukizi yanayotokana na uchafu.

Hata hivyo Kihwelo alishukuru klabu ya Rotary kwa kutoa msaada wa vioski vya maji katika milango ya Hospitali ya Wazazi ya Meta na Hospitali ya Rufaa ambavyo vinasaidia watu wanaoingia na kutoka kuvitumia kunawa ambapo Hospitali inahudumia Sabuni za kunawia bila kukosa.

Kwa upande wake Mgeni Rasmi Adrian Majembe amesema kuwa jukumu la kunawa mikono lisiishie kwa wageni wanaoingia na kutoka Hospitali bali pia wauguzi nao wanalo jukumu la kunawa  kabla na baada pindi wanapowahudumia wagonjwa Hospitalini.

Pia Majembe ambaye ni mmoja wa wadau wakubwa wa Sekta ya Afya amesema kuwa hivi sasa wametoa elimu kwa wanafunzi zaidi ya 1000 Jijini Mbeya na maeneo ya Masoko na ujumbe huo kupokewa vizuri ambapo umetoa matokeo mazuri.

Hivyo amewataka wakazi wa Mbeya kuendelea kusambaza ujumbe huu ili kuendelea kupunguza idadi ya wagonjwa wanaotokana na kutonawa mikono.

Majembe amewashukuru klabu ya Rotary kwa msaada wao wa hali na mali ambapo katika sherehe hizo klabu hiyo iliwakilishwa na Rais Mstaafu wa Mkoa Ephraim Njuu na Rais wa Mkoa wa sasa Melas Mdemu amabao waeahidi kusaidia Serikali nafasi inapopatikana. 

Na Mbeya yetu

No comments: