Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, May 6, 2014

NMB YATOA MAADA WA VITU MBALIMBALI KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO KYELA


 Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Magreth Ester Malenga,  akipokea msaada wa vitu mbali mbali kutoka Benki ya NMB Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Lucresia Makiriye,na meneja NMB tawi la Kyela Hamadan Silliah wakati wakikabidhi misaada hiyo




 Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Magreth Malenga akimshukuru Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Lucresia Makiriye, Kwa benki ya NMB kwa msaada walioutoa

 Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Magreth Malenga alisema hivi sasa hakuna mwananchi atakayekuwa na shida ya chakula na kwamba atahakikisha walengwa wanafikishiwa kama ilivyokusudiwa.


 Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Lucresia Makiriye, alisema benki yao imeguswa sana na maafa yaliyotokea hivyo wameamua kutoa msaada kwa waathirika ili waweze kuishi kama Watanzania wengine.









ZAIDI ya Shilingi Bilioni 2.3 zinahitajika kwa ajili ya kurudisha miundombinu ya barabara za Halmashauri ya Wilaya ya Kyela baada ya kuharibiwa vibaya na mafuriko yaliyoikumba Wilaya hiyo hivi karibuni.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Magreth Ester Malenga, alipokuwa akitoa tathmini ya athari zilizotokana na mafuriko wakati akipokea msaada wa vitu mbali mbali kutoka Benki ya NMB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.

Malenga alisema miundombinu ya barabara katika kuvifikia vijiji ni mibaya na haipitiki kabisa hali inayosababisha baadhi ya waathirika wa mafuriko kutofikiwa kwa wakati hivyo ili iweze kurudi katika hali yake ya kawaida zinahitajika kiasi hicho cha Shilingi Bilioni 2.3 kwa barabara za Halmashauri pekee.

Alisema katika mafuriko hayo hadi sasa Watu 7 wamepoteza maisha huku mwili mmoja ukiwa haujapatikana kutokana na kusombwa na maji na kaya 3983 ndizo zilizokumbwa na athari ya mafuriko hayo.

Aliongeza kuwa kati ya kaya hizo ni kaya 235 zenye wakazi 1080 ndizo zilizoathirika kwa kiasi kikubwa sana ingawa zimepata misaada mbali mbali kutoka Serikalini, Mashirika binafsi na watu mbali mbali.

Alisema msaada zaidi unahitajika kwa ajili ya kuzifikia kaya zingine 2040 ambazo bado hazipatiwa msaada wowote wa chakula na mahitaji ya kawaida kutokana na miundombinu kuwa mibovu ya kuwafikia walipo.

Mkuu huyo wa Wilaya aliongeza kuwa tangu kutokea kwa maafa hayo Serikali imetoa Tani 6 za Mahindi pamoja na fedha za kusagia na kununulia maharage kwa ajili ya waathirika huku mwananchi mmoja mmoja akijitokeza kuchangia alichonacho pamoja na mashirika.

Kwa upande wake Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Lucresia Makiriye, alisema benki yao imeguswa sana na maafa yaliyotokea hivyo wameamua kutoa msaada kwa waathirika ili waweze kuishi kama Watanzania wengine.

Alisema NMB imetoa vitu vya thamani ya Shilingi Milioni 10 pamoja na kusafirisha hadi wilayani Kyela ambavyo vitazinufaisha kaya zaidi ya 320 zilizopatwa na majanga ya mafuriko hayo.

Alivitaja vitu hivyo kuwa ni pamoja na Mchele kilo 3200 ambao utagawiwa kwa kilo kumi kwa kila kaya, Maharage kilo 1600 kila kaya kilo 5 na  mafuta ya kupikia Katoni 54 ambapo kila kaya itapata Lita tatu.

Akishukuru kwa ajili ya msaada huo Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Magreth Malenga alisema hivi sasa hakuna mwananchi atakayekuwa na shida ya chakula na kwamba atahakikisha walengwa wanafikishiwa kama ilivyokusudiwa.

Mwisho.

Na Mbeya yetu

No comments: