Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, May 6, 2014

MAADHIMISHO YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI MKOA WA MBEYA YAFANA.

Raisi Mstaafu wa Muungano wa Klabu za waandishi wa habari(UTPC), Ulimboka Mwakilili, alipokuwa akizungumza katika sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya habari duniani zilizoadhimishwa kwa Mkoa wa Mbeya kwenye ukumbi wa Itemba Green Village uliopo Ilomba jijini Mbeya.

 Mwenyekiti wa Klabu wa Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya, Uswege Luhanga, alisema waandishi wanapaswa kuwa na umoja na mshikamano ili kuweza kujiletea maendeleo yao na klabu kwa ujumla.


Mwandishi mkongwe Meshack Njavike akisalimia vijana wake katika sherehe hizo

Ni vigeregere na vifijo tu ukumbini





















WAANDISHI wa habari nchini wametakiwa kuwa na vyanzo vingine vya mapato badala ya kutegemea shughuli za uandishi pekee ili kuwa na urithi kwa familia zao na vizazi vijavyo.

Wito huo ulitolewa na Raisi Mstaafu wa Muungano wa Klabu za waandishi wa habari(UTPC), Ulimboka Mwakilili, alipokuwa akizungumza katika sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya habari duniani zilizoadhimishwa kwa Mkoa wa Mbeya kwenye ukumbi wa Itemba Green Village uliopo Ilomba jijini Mbeya.

Mwakilili ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo zilizofana kupita kawaida alisema waandishi wa habari wanapaswa kuwa wabunifu wa kuwa na miradi mingine itakayowasaidia kuongeza vipato vyao na siyo kukaa na kusubiri posho kutoka kwa wadau.

Alisema wadau pia wanapaswa kuheshimu kazi za waandishi wa habari kwa kuwatumia inavyotakiwa kwa kuzingatia maadili na sheria za Nchi na siyo kumtumia mwandishi kwa maslahi binafsi.

Kwa upande wake Mgeni mashuhuri wa sherehe hizo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, alipongeza chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya(MBPC) kwa kumheshimu na kumshirikisha katika sherehe hizo.

Alisema ataendelea kushirikiana na vyombo vyombo vya habari Mkoa wa Mbeya ili kuhakikisha hali ya amani na utulivu inaimarika ndani ya Mkoa na kuufanya kuwa kivutio cha wageni na wawekezaji.

Awali akimkaribisha Mgeni rasmi, Mwenyekiti wa Klabu wa Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya, Uswege Luhanga, alisema waandishi wanapaswa kuwa na umoja na mshikamano ili kuweza kujiletea maendeleo yao na klabu kwa ujumla.

Katika maadhimisho hayo, Klabu ya waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya ilifanya sherehe zake kwa kutanguliwa na bonanza kubwa la michezo lililofanyika katika viwanja vya Chuo cha Uhasibu (TIA) Mafiati Mwanjelwa jijini Mbeya na baadaye sherehe ya Jioni kwenye Ukumbi wa Itemba.

Akizungumzia Bonanza hilo, Mratibu wa Sherehe hizo, Venance Matinya, alisema michezo mbali mbali ilichezwa na washindi kukabidhiwa zawadi kutoka kwa viongozi wa Mbeya Press.

Aliitaja michezo hiyo kuwa ni pamoja na mpira wa miguu ambao Timu ya Chama cha Wasanii Mkoa wa mbeya waliibuka kidedea na kujinyakulia fedha taslimu shilingi Elfu hamsini(50,000/=), Mpira wa Pete walishinda timu ya Kabwe Queens waliojinyakulia 20,000/=.

Michezo mingine ni kuvuta kamba, kukimbiza kuku, kukimbia kwenye magunia, kutembea na yai na kuokota Fedha.

Mwisho.

Na Mbeya yetu




No comments: