Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Monday, May 26, 2014

KITUO CHA NURU OPHANS CHAKABIDHI VITENDEA KAZI KWA VIJANA WANAOISHI KWENYE MAZINGIRA MAGUMU MBEYA

 Venance Matinya kutoka  mtandao wa Mbeya yetu Blog  akipokea Hati ya shukrani kutoka kwa Mgeni Rasmi Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Mbeya, Thobias Mwalwego kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa kwa kutambua mchango wa Mbeya yetu  Blog katika kulea watoto yatima

 mwanafunzi aliyehitimu fani ya ufundi wa magari akikabidhiwa vifaa vyake.
 Mwanafunzi aliyehitimu fani ya kilimo cha mbaogamboga akikabidhiwa vitendea kazi.
 Mwanafunzi wa fani ya useremala naye akikabidhiwa vitendea kazi.
 Mgeni rasmi, Afisa ustawi wa jamii Mkoa wa Mbeya, Thobias Mwalwego akihutubia katika hafla hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro.


Mwanafunzi wa fani ya ushonaji akikabidhiwa vitendea kazi ambacho ni Cherehani.
  Meneja wa Kituo, Amanda Fihavango akiwaeleza jambo waandishi wa habari
.Mkurugenzi wa Nuru Orphans centre Jasson Fihavango akisoma risala.
 Mwanafunzi akikabidhiwa cheti cha kuhitimu masomo yake.
Wageni waalikwa wakitembelea majengo ya kituo cha nuru.

KITUO cha Nuru Ophans kimekabidhi vitendea kazi kwa vijana wanaoishi kwenye mazingira magumu Mbeya baada ya kuhitimu mafunzo ya fani mbali mbali kutoka Chuo cha ufundi Veta mkoani Mbeya.
 
Hafla hiyo ilifanyika juzi katika makao makuu ya kituo hicho kilichopo Uyole Jijini Mbeya ambapo vijana 30 walipewa vyeti vya kuhitimu masomo yao pamoja na vifaa vya kufanyia kazi.
 
Meneja Miradi wa Nuru Ophans Centre, Osward Poyo,alisema Asasi yake baada ya kufanya utafiti ilibaini kuwepo kwa vijana wanaoishi katika mazingira magumu  2500 katika kata 6.
 
Alisema baada ya kubaini hayo Asasi hiyo iliomba msaada kwa Ubalozi wa Marekani nchini kwa ajili ya kuwasomesha vijana hao fani mbali mbali za ufundi lakini Ubalozi ulikubali kuwasomesha vijana 30 tu hivyo kufanya kila kata kutoa vijana 5.
 
Aliongeza kuwa Ubalozi wa Marekani baada ya kutiliana sahihi mkataba wa kuwasomesha vijana hao walitoa jumla ya shilingi 16,800,000 kwa malipo ya ada, Nauli ya kwenda na kurudi chuoni, malipo ya chakula kwa siku zote za masomo na ununuzi wa Vitendea kazi kulingana na fani ambazo vijana wamesomea.
 
Alizitaja fani ambazo vijana hao wamesomea na vifaa walivyokabidhiwa kuwa ni pamoja na fani ya Ushonaji ambayo ilikuwa na vijana 12 waliokabidhiwa Cherehani kila mmoja,Seremala kijana mmoja aliyekabidhiwa Misumeno 3,Landa 2, Nyundo pamoja na Ovaroli.
 
Wengine ni fani za Ufundi magari ambao ulikuwa na vijana 6 ambao kila mmoja alikabidhiwa Ovaroli,dazani ya spana na Jeki ya kuinulia magari na vijana 9 waliochukua fani ya udereva ambao walipewa Leseni za kuendeshea magari na vijana wawili waliosoma fani ya klilimo cha mboga mboga ambao walipewa kila mmoja kilo 50 za mbolea aina ya Urea, Mbegu za mahindi kilo 6, Pumpu ya kunyunyizia dawa 1 pamoja na mbegu za mboga za nyanya, spinachi na karoti.
 
Naye Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Afisa ustawi wa jamii Mkoa wa Mbeya,Thobias Mwalwego, ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, alitoa wito kwa vijana wa fani za ufundi kuwa waaminifu kwa wateja wao na huduma watakazokuwa wakitoa kwa manufaa ya jamii nzima.
 
Alisema vifaa walivyokabidhiwa vinafaa kutunzwa na siyo kukimbilia kuuza hali ambayo inaweza kuwarudisha katika hali ya awali ya kuzurura mitaani bila kuwa na fani ya kufanya.

Na Mbeya yetu Blog

 

No comments: