Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, April 15, 2014

WENDA MABINGWA WAPYA WA LIGI YA MKOA WA MBEYA, YASHINDA MECHI ZOTE HATUA YA SITA BORA

Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari ya Wenda Fidelis Mwampoma ambaye pia ni mmiliki wa Timu ya Mpira wa miguu ya Wenda akizungumzia ushindi wa timu yake baada ya kuibuka mshindi wa ligi ya Mkoa wa Mbeya.

Kapteni wa timu ya Wenda akizungumza kwa furaha baada ya timu yake kuishinda timu ya Sido goli mbili kwa moja katika fainali za kumtafuta bingwa wa ligi ya Mkoa wa Mbeya.

Mkurugenzi wa Wenda Sekondari akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji na mashabiki wa timu hiyo.

Baadhi ya mashabiki wa timu ya Wenda wakishangilia baada ya mpira kumalizika


Wachezaji na mashabiki wa Wenda wakiendelea kushangilia kuwa mabingwa wa ligi ya Mkoa wa Mbeya

Wachezaji wa akiba wa timu ya Sido ya jijini Mbeya wakifuatilia kwa makini mchezo ukiendelea


Mtanange ukiendelea katika uwanja wa Jeshi Mbalizi

Katibu wa Mrefa Suleiman Haroub pamoja na wasimamizi wa ligi wakifuatilia kwa makini mchezo huo



Wazee wa kazi wakiwa vitani na lazima mshindi apatikane.



TIMU ya Mpira wa miguu ya Wenda yenye makao yake makuu Mbalizi Wilaya ya Mbeya mkoani hapa imefanikiwa kuibuka bingwa wa ligi ya Mkoa wa Mbeya baada ya kuibwaga Timu ya Sido ya jijini Mbeya katika fainali iliyopigwa mwishoni mwa wiki katika Uwanja wa Jeshi Mbalizi.

Timu ya Wenda iliibuka kidedea na kuwa bingwa wa Mkoa wa Mbeya baada ya kuibuka na magoli mawili kwa moja dhidi ya Timu ya Sido ambapo magoli ya timu ya Wenda yalifungwa na Ally Kheri dakika ya 11 ya mchezo kwa adhabu ndogo iliyojaa wavuni moja kwa moja.

Dakika ya 48 ya mchezo huo Bahati Mwashiuya aliifungia timu yake goli la pili baada ya kuwazidi kasi walinzi wa timu ya Sidon a kuwafanya washambuliaji wa Timu ya Sido kuongeza kasi wakitaka kusawazisha magoli hayo na hatimaye kuibuka na ushindi.

Kasi ya washambuliaji wa Sido ilizaa matunda katika dakika ya 85 ya Mchezo huo baada ya Mshambuliaji wake Daniel Peter kuangushwa katika eneo la hatari wakati akielekea kumsabahi Mlinda ,mlango wa Wenda na hivyo Mwamuzi wa kati Ngole Mwangole kuamuru Mkwaju wa penati upigwe.

Aidha mkwaju wa penati uliopigwa kiufundi na Meja Mgome uliiandikia goli la kufutia machozi timu ya Sido lililodumu hadi kipenga cha mwisho kutoka kwa mwamuzi Ngole Mwangole kutoka jijini Mbeya Timu ya Wenda 2 na Sido 1.

Kwa upande wake mmiliki wa Timu ya Wenda ambaye pia ni Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari ya Wenda na Mkuu wa Shule ya Sekondari Mbalizi, Fidelis Mwampoma alisema matokeo hayo ni maandalizi mazuri ya timu yake ambayo haijafungwa tangu kuingia katika mzunguko wa sita bora.

Alizitaja timu ilizoingia nazo katika mzunguko huo na kushinda zote kuwa ni pamoja na Mchezo kati ya timu yake na Biashara fc kutoka Chunya ambapo waliibuka kwa goli moja bila kitu, Dhidi ya Tukuyu Star mabingwa wa ligi kuu wazamani  Moja kwa sifuri, Mazombe fc kutoka Kyela goli 2 kwa moja, Airport fc kutoka jijini Mbeya magoli matatu kwa moja na Sido iliyotinga fainali iliyotokanayo Mbili kwa Moja.

Aliongeza kuwa ushindi huo unarudisha furaha kwa mashabiki wa Wilaya ya Mbeya iliyopotea tangu miaka ya 1997 ambapo Wilaya hiyo haikuwahi kutoa bingwa wa Mkoa wa Mbeya ambapo timu zilikuwa zikitoka kwenye wilaya zingine.

Alisema mikakati yao ni kuhakikisha timu ya Wenda inacheza ligi kuu na kufanya Mkoa wa Mbeya kuwa timu nyingine tishio kama ilivyo Mbeya City inayomilikiwa na Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Mwisho.

Na Mbeya yetu

No comments: