Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Monday, April 28, 2014

LIGI ya Kombe la Bodaboda Jiji la Mbeya inatarajia kuanza kutimua vumbi Mei 3, Mwaka huu ikizishirikisha timu za waendesha pikipiki maarufu kwa jina la Bodaboda Jijini Mbeya

Mmoja wa wakurugenzi wa kampuni Kampuni ya Citysign Promotion & Markerting Agency Limited ya Jijini Mbeya Geophrey Mwangunguru katika kikao cha maandalizi baina yao na viongozi wa chama cha waendesha bodaboda kilichofanyika katika viwanja vya City pub Jijini Mbeya alisema ligi hiyo itakuwa na timu 16 ambazo zitatoka katika kanda sita za bodaboda jijini Mbeya. 


Mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa shirikisho la mpira wa miguu Jiji la Mbeya(MUFA) Ramadhani Lulandala alisema ni vema madereva wa bodaboda wakajiandaa vizuri huku wakitambua sheria na kanuni za mpira wa miguu kwa kuepuka kuwafanyia vurugu waamuzi na kwamba atakayebainika atachukuliwa hatua kali za kisheria.






LIGI ya Kombe la Bodaboda Jiji la Mbeya inatarajia kuanza kutimua vumbi Mei 3, Mwaka huu ikizishirikisha timu za waendesha pikipiki maarufu kwa jina la Bodaboda kwenye viwanja vya shule ya Msingi Mwenge.

Ligi hiyo imeandaliwa na kampuni ya Citysign Promotion and Marketing Agency yenye makao makuu jijini Mbeya ikishirikiana na wadau mbali mbali wapenda michezo pamoja na chama cha Mpira wa Miguu Jiji la Mbeya(MUFA).

Akizungumza kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya ligi hiyo, mmoja wa Viongozi wa Kampuni hiyo, Geophrey Mwangunguru, alisema tayari timu 16 zimethibitisha kushiriki ligi hiyo baada ya kukamilisha kujaza fomu maalumu zinazotumiwa na TFF.

Alisema timu hizo zitagawanywa katika makundi manne ambapo kila kundi litakuwa na timu nne zitakazo chezwa mara nne kwa wiki kutokana na  kutumika kwa kiwanja kimoja cha Mwenge Shule ya Msingi kilichopo Soweto jijini hapa.

Aidha alizitaja zawadi ambazo washindi watajinyakulia ni kwa mshindi wa kwanza atakaeibuka na pikipiki moja mpya huku mshindi wa pili akijipatia fedha taslimu shilingi Laki saba na mshindi wa tatu akiondoka na shilingi Laki tatu taslimu.

Kwa upande wake Mratibu wa Ligi hiyo kutoka kampuni ya Citysign Promotion, Charles Mwanjisi, alisema lengo la kuandaa ligi kwa ajili ya madereva wa boda boda ni kuwakutanisha na jamii ili kuondoa dhana potofu ya kwamba bodaboda ni wahuni pamoja na kutoa burudani.

Nao baadhi ya viongozi wa timu hizo waliishukuru kampuni hiyo kwa kuwakumbuku na kuwathamini kama na wao ni watu ndani ya jamii kwa kuwaandalia ligi ambayo itachangia kufahamiana miongoni mwa jamii na madereva.

Walisema ni lazima washiriki ligi hiyo kikamilifu ili kuwatia nguvu waandaaji ili washawishike na siku nyingi kutokana na mwitikio watakaoupata kutoka kwa washiriki wa ligi hiyo ambao ni madereva wa pikipiki.

Mwisho.

Na Mbeya yetu

No comments: