Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Monday, April 28, 2014

TANGAZO LA KUPOTEA KWA MTOTO SABRINA ATHUMAN 11 NI MWANAFUNZI SHULE YA MSINGI KAGERA MBEYA

Pichani ni Mtoto Sabrina Athuman (11)aliyepotea



Na Esther Macha, Mbeya

MWANAFUNZI  aliyefahamika kwa jina la Sabrina  Athuman (11) anayesoma darasa la nne katika shule ya Msingi Kagera iliyopo kata ya Ilomba Jijini Mbeya  ametoweka nyumbani kwao  katika mazingira ya kutatanisha toka April 26 mwaka huu .

Akizungumza na Mbeya yetu  ,Baba Mlezi wa mtoto huyo, Jumbe Said Zungiza alisema kuwa  mtoto huyo alitoweka nyumbani  kwao eneo la Mama John  April 26 mwaka huu majira ya saa 1.00 asubuhi bila kuaga.

“Kawaida huwa tunajua kuwa mtoto wetu siku za jumamosi huwa anaenda shuleni kwenye mitihani  na kabla hajaenda shule kawaida huwa tunampa sh.500 ya mtihani lakini cha kushangaza siku hiyo tulishtuka kuona hayupo na kitendo cha kutoaga kilituchanganya ikabidi tuingie chumbani kwake lakin hatukufanikiwa kumuona  mpaka sasa”alisema Baba wa mtoto huyo.

Akizungumzia kuhusu mazingira ya kupotea kwa mtoto huyo Bw.Zungiza alisema kuwa mazingira aliyoondoka mtoto huyo yanazidi kuwapa wasiwasi kwani aliondoka asubuhi sana na kilichowafanya wazazi hao kushtuka ni baada ya kuamka kuona milango ya nje ipo wazi ndipo walipoanza kuita na hakuitika.

Aliiongeza kuwa walimtafuta mtoto huyo  mpaka kufika shuleni kwao ambako nako hakufika kufanya mitihani na ndipo zilipoanza juhudi za kutoa taarifa  polisi,Misikitini lakini hajaweza  kupatikana licha ya juhudi zote kufanyika kwa kushirikiana na ndugu  na marafiki .

Kwa upande wake Mama mlezi wa Mtoto huyo Riziki Jumbe alisema April 26 mwaka siku alipotoweka mtoto huyo nyumbani alivaa SURUALI ya KAKI ,SWETA yenye rangi mchanganyiko ambayo ni Nyekundu,Kijani ,Bluu,pamoja na kuvaa Hijabu kichwani Nyeupe.

Aidha Bi.Jumbe alisema kwamba rangi ya mtoto huyo ni Maji ya kunde ,na mrefu mwemba mwemba  na kwamba mara nyingi anapenda kutembelea  maeneo ya Mswiswi  kwa mjomba wake lakini huko hajaweza kufika..

Kwa yeyote mwenye taarifa za mtoto huyo awasiliane na Baba Mlezi wa Mtoto huyo Jumbe Said Zungiza kwa namba 0767810191 au 0715810191, Mama Mlezi  Riziki Jumbe 0756684016

No comments: