Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, March 25, 2014

SIKU YA HALI YA HEWA DUNIANI UJUMBE WATOLEWA KWA VIJANA


Meneja wa Kanda ya Nyanda za juu kusini magharibi wa Mamlaka ya hali ya hewa, Ahmed Issa, alipokuwa akizungumza na wanafunzi wa Shule ya sekondari Wenda walipotembelea kituo hicho katika kuadhimisha siku ya hali ya hewa duniani.

Wanafunzi wa Shule ya sekondari Wenda wakimsikiliza Meneja wa mamlaka ya hali ya hewa


Baadhia ya waalimu na wadau mbali mbali wa jijini Mbeya walihudhuria 


Baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya hali ya hewa nyanda za juu kusini wakiwa makini kumsikiliza meneja wako katika siku hiyo ya hali ya hewa Duniani

Wanafunzi wa shule ya Sekondari Wenda wakipata somo fupi la hali ya hewa













SERIKALI imetakiwa kutoa mitaala ya elimu kuhusu hali ya hewa katika shule za Sekondari nchini ili kukabiliana na ongezeko la joto na mabadiliko ya tabia ya nchi katika karne zijazo.

wito huo ulitolewa  na Meneja wa Kanda ya Nyanda za juu kusini magharibi wa Mamlaka ya hali ya hewa, Ahmed Issa, alipokuwa akizungumza na wanafunzi wa Shule ya sekondari Wenda walipotembelea kituo hicho katika kuadhimisha siku ya hali ya hewa duniani.

Alisema kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni mabadiliko ya hali ya hewa na vijana hivyo ni muhimu kwa Serikali kuandaa mitaala ya elimu kuhusiana na hali ya hewa ili kuwafanya vijana waelewe njia mbali mbali za kukabiliana na ongezeko hilo kwa miaka ya baadaye kwa kuwa ndiyo watakaokuwepo.

“ Vijana ndiyo watakaokuwepo na kuishi katika karne zijazo, hivyo ni bora tukajikita katika kuwaelimisha wao kwa serikali kuandaa mitaala ya masomo wakiwa mashuleni namna ya kuendana na mabadiliko yanayotokea” alisema meneja huyo.

Aliongeza kuwa tangu mwaka 1850 kumekuwa na kasi ndogo ya mabadiliko ya hali ya hewa kwa joto kuongezeka duniani lakini kadiri muda unavyoozidi kusonga mbele joto linazidi kuongezeka hadi kufikia asilimia 0.75 hadi asilimia moja na utabiri ukionyesha hali kuwa mbaya zaidi.

Alisema hadi sasa zaidi ya asilimia 60 ya ongezeko la joto duniani husababishwa na hewa mkaa angani ambapo njia kuu ya kukabiliana na hali hiyo ni pamoja na upandaji wa miti ya asili kuendana na eneo husika itakayochangia kunyesha kwa mvua yenye manufaa katika jamii.

Meneja huyo alisema hayo yote yanawezekana kukabiliana nayo ikiwa ni kushirikisha vijana na kuwapa elimu mapema na kuzingatia umuhimu wa ufuatiliaji wa taarifa zinazotolewa na mamlaka ya hali ya hewa na jinsi ya kujihami.

Mwisho.

Na Mbeya yetu

No comments: