Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, January 29, 2014

SHIRIKA LA NYUMBA MBEYA LAMFUNGIA MPANGAJI WAKE NDANI YA DUKA PAMOJA NA WAFANYAKAZI.


Akizungumzia Dirishani kufuatia kufungiwa kwa duka lake na yeye akiwa ndani pamoja na wafanyakazi wake wawili, Mmiliki wa Duka hilo, Boniface Ishabakaki, alisema ameshangaa kufanyika kwa kitendo hicho kwa sababu tayari Mke wake alikuwa ameshaongea na Meneja na kumtumia Fedha kwa njia ya Mpesa tangu saa nne lakini alivyowaeleza walishindwa kumuelewa.


Mzee Boniface Ishabakaki(Lubi),  na Cecilia wakiwaonesha waandishi wa habari majina yao kuptia dirisha la kioo wakiwa wamefungiwa na shirika la nyumba.





 Afisa wa shirika la Nyumba mkoani Mbeya, Alfan Chaula, baada ya kufungua kufuli  akiwa anawakwepa wana habari


Mmiliki wa Duka hilo, Boniface Ishabakaki, akiongea na waandishi wa habari baada ya kufunguliwa duka lake


Kaimu Meneja wa shirika la Nyumba mkoa wa Mbeya S.C Katanga akifafanua swala la kufungiwa kwa mfanyabiashara huyo



Amos Manyama Afisa Miliki wa shirika la nyumba akielezea mikakati ya shirika hilo kwa waandishi wa habari 

Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa makini kuwasikiliza maafisa hao wa shirika la nyumba




Katika hali isiyokuwa ya Kawaida Shirika la Nyumba la Taifa(NHC) Mkoa Mbeya limemfungia mpangaji wake ndani ya duka katika kile kilichodaiwa kuchelewa kulipia pango la chumba hicho kwa muda uliokusudiwa ambao ni Mwanzo wa Mwezi.

Tukio hilo ambalo lilivuta hisia za Watu wengi kutokana na afya ya Mpangaji huyo anayesumbuliwa na Kisukari kwa Muda mrefu limetokea Leo majira ya saa nne kati kati ya Jiji la Mbeya ambapo Watumishi wa Shirika hilo walifunga Duka la Kuuzia vifaa vya Maofisini(Stationary) inayojulikana kwa jila la Rubi iliyopo Posta.

Akizungumzia Dirishani kufuatia kufungiwa kwa duka lake na yeye akiwa ndani pamoja na wafanyakazi wake wawili, Mmiliki wa Duka hilo, Boniface Ishabakaki, alisema ameshangaa kufanyika kwa kitendo hicho kwa sababu tayari Mke wake alikuwa ameshaongea na Meneja na kumtumia Fedha kwa njia ya Mpesa tangu saa nne lakini alivyowaeleza walishindwa kumuelewa.

Hata hivyo baadhi ya watu walioshuhudia kitendo hicho wamelaani vikali kwa kile walichodai Shirika hilo limegeuka adui wa wapangaji wao ambao hata hivyo hawana madeni ya kutisha na siyo wasumbufu kwenye ulipaji na kuongeza kuwa mzee huyo amekuwa mpangaji wa shirika hilo tangu Mwaka 2000.

Walisema kitendo cha kumfungia mtu dukani au chumbani ni hatari kutokana na majanga ya moto kuibuka pasip taarifa hivyo kama mtu yuko ndani na majanga yametokea ni vipi wanaweza kumuokoa ili hali amefungiwa nje na kuongeza kuwa mgonjwa wa kisukari kawaida anahitaji kwenda katika haja ndogo kila mara.

Aidha kutokana na kelele za baadhi ya waandishi waliofika katika hilo na kulazimu kupiga Simu Polisi ambapo muda mfupi baadaye alionekana mmoja wa wafanyakazi wa Shirika hilo ambaye hakutaka kuzungumzia ishu yoyote alijitokeza na kufungua Duka hilo na kutokomea.

Kwa upande wakeKaimu Meneja wa shirika la Nyumba mkoa wa Mbeya S.C Katanga amesema Ndugu Ishabakaki ni mpangaji wao wa nyumba Na. 003 Kiwanja Na. 6/3 Mtaa wa Lupaway. Mbali na jitihada zote za kumdai kodi amekuwa msumbufu kulipa pia historia yake ya ulipaji kodi si mzuri hata kulifikisha shirika katika hatua ya kutoa Notisi na wakati mwingine kumpeleka Dalali.

Aidha kwa mwezi January 2014 Ishabakaki  alipewa Demand Note iliyomtaka alipe kodi yake yote ya Tsh 222,450, ndani ya juma la kwanza la mwezi na hakutekeleza wajibu wakehuo.

Shirika liliendelea kumkumbusha ambapo tarehe 18, 22, na 27 alitembelewa na maafisa wa shirika kumkumbusha na bado akashindwa kutekeleza wajibu huo.

Mnamo tatehe 29/01/2014 shirika liliamua kufunga sehemu ya Ishabakaki kwa muda ili kumhamasisha alipe deni na kweli baada ya kufungiwa alilipa deni hilo lote la Tsh 222,450.00

Na Mbeya yetu

No comments: