Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, January 29, 2014

CHAMA cha Mapinduzi(CCM) kimesema kinajivunia msingi uliojiwekea wa kukua kwa uchumi tangu kuzaliwa kwa chama hicho Mwaka 1977, ambapo matokeo na matunda yake yataanza kuonekana hivi sasa.


Katibu wa Siasa, Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nauye, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika katika Ofisi za Chama hicho Mkoa wa Mbeya kuhusiana na Sherehe za kuadhimisha miaka 37 tangu kuzaliwa kwa chama zitakazofanyika Kitaifa Mkoani Mbeya.

Baadhi ya waandishi wa habari wa mkoa wa Mbeya wakimsikiliza Nape nauye







CHAMA cha Mapinduzi(CCM) kimesema kinajivunia msingi uliojiwekea wa kukua kwa uchumi tangu kuzaliwa kwa chama hicho Mwaka 1977, ambapo matokeo na matunda yake yataanza kuonekana hivi sasa.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu wa Siasa, Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nauye, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika katika Ofisi za Chama hicho Mkoa wa Mbeya kuhusiana na Sherehe za kuadhimisha miaka 37 tangu kuzaliwa kwa chama zitakazofanyika Kitaifa Mkoani Mbeya.

Nape alisema katika maadhimisho ya kuzaliwa kwa CCM, Wanavijivunia mafanikio mengi ikiwemo msingi uliojengwa wa kukua kwa uchumi wa Nchi ambapo matokeo yake yataanza kuonekana hivi karibuni kwa Watanzania kufaidi matunda yaliwekwa na Chama tawala.

Aidha aliwataka Watanzania na Wakazi wa Mkoa wa Mbeya kujitokeza kwa wingi kumlaki Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa na mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ambayo yatatanguliwa na Matembezi ya mshikamano.

Katibu huyo aliongeza kuwa Maadhimisho ya Miaka 37 tangu kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi huadhimishwa kila Tarehe 5 ya kila Mwaka lakini mwaka huu sherehe hizo zimerudishwa nyuma na kufanyika Februari 2, Mwaka huu kwa kile alichodai ni kupisha siku za kazi ili wananchi wajikite katika shughuli za uzalishaji mali.

Alisema Viongozi wa Kitaifa wameshaanza kuwasili ambapo Katibu Mkuu wa Chama hicho atawahi kufika akifuatiwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa bara kabla ya kumpokea Raisi Februari Mosi tayari kwa Sherehe za Tarehe 2 Februari Mwaka huu.

Alisema kabla ya Sherehe viongozi wa Chama kitafanya shughuli mbali mbali za maendeleo ambazo ni kushiriki kazi za kijamii kama ujenzi wa vyumba vya madarasa, ujenzi wa zahanati, usafi wa Mazingira pamoja na kupanda miti kwenye vyanzo vya maji ndani ya Jiji la Mbeya.

Nape aliongeza kuwa Sherehe hizo zilifunguliwa rasmi Januari 26, Mwaka huu na Makamu Mwenyekiti wa CCM Visiwani ambaye pia ni Raisi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk. Mahamed Shein kisha kusherekewa katika kila ngazi kuanzia vitongoji, vijiji, Wilaya n Mikoa Nchi nzima.

Alisema katika sherehe hizo ambazo zitaanza na matembezi ya Mshikamano yatakayoongozwa na Mheshimiwa Raisi kuanzia ,majira ya saa Mbili asubuhi yatakayoanzia Soweto na Kuishia makao makuu ya Ofisi za chama Mkoa na baadaye kuendelea na Sherehe katika Uwanja wa Sokoine kuanzia majira ya saa nane mchana zikipambwa na burudani mbali mbali zikiongozwa na Bendi ya TOT.

Na Mbeya yetu

1 comment:

Anonymous said...

TUMEFANIKIWA KUONDOA DIVISHENI ZIRO NA SASA TUNA DIVISHENI TANO, VERY GOOD CCM.