Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, January 17, 2014

MSIMU WA MVUA WATU WANUFAIKA NA KUMBIKUMBI


Wengi wetu tumekuwa tukisikia kuwa kuna wadudu watamu sana na hupatikana sana hasa katika msimu wa Mvua, wadudu hao ambao ni Maarufu kwa jina la Kumbikumbi huanza kujitokeza wakati wa mvua hasa katika vichuguu vyao vikubwa ambavyo hufaamika kwa kuishi wadudu wengine wanaojulikana kwa jina la mchwa hawa hugeuka na kuja kuwa kumbikumbi.

Mkoa wa Mbeya ni moja ya maeneo ambayo kunapatikana kumbikumbi kwa wingi sana ..Kupitia ukurasa huu wa  Mbeya yetu blog leo tutapata kujionea jinsi kumbikumbi hao wanavyopatikana.
 Hiki ni kichuguu ambacho kimefunikwa kwa umahili kabisa, ambapo kote hakuna mwanga isipokuwa sehemu moja tuu.

 Hili ni Tundu dogo maalumambapo kumbikumbi hawa hupumbazika na mwanga huu wakijua kuna mwanga ili watoke na ndipo wanapo kamatwa 
 Hii ni ndoo ambayo imetegeshwa katika Tundu dogo ambapo panatoka Mwanga , hapa ndipo kumbikumbi hawa wanapotokea na kudumbukia katika ndoo hiyo na hatimaye kushindwa pa kutokea 

Picha hii inaonesha Jinsi kumbikumbi waliochanganyikana na Mchwa wakiwa wamedondokea katika Ndoo maalum ambayo hapa ni mtego wa kuwatega Kumbikumbi hawa.
 Anaitwa Bwana Edward ambaye ni mtaalam wa kuandaa vichuguu hivyo, hapa alikuwa akihakikisha kama kweli kuna kumbikumbi hao.

 Hii ni aina tofauti ya Kichuguu ambacho kimejitokeza pembezoni mwa shamba.
 Huu ni aina nyengine ya mtego wa kumbikumbi hao 

Hii ni Njia ambayo kumbikumbi hao wanakuwa wakitokea huku wakifuata mwanga  watoke na kujikuta wapo mtegoni.
Juu ni vichuguu ambavyo bado havijatengenezwa , vikiwa vinaandaliwa kwa ajili ya kuwatega kumbikumbi hao..

Picha zote na Mbeya yetu blog

No comments: