Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, January 21, 2014

ALIYEJIFUNGUA MAPACHA WANNE AZIDI KUPEWA MISAADA.









WADAU mbali mbali na wasamaria wema wamezidi kujitokeza kumpa msaada wa hali na Mali,Aida Nakawala(25) mkazi wa kijiji cha Chiwanda Wilaya ya Momba Mkoa wa Mbeya, aliyejifungua watoto wanne  mapacha kwa mkupuo(Quadruplets) katika usiku wa kuamkia Mwaka mpya.

Misaada hiyo imeongozana ikiwa ni siku moja baada ya Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari Vanesa pamoja na Mbeya yetu kutoa misaada mbali mbali ambapo leo Kampuni ya Arif Electronic nayo imeguswa.

Mkurugenzi wa Kampuni hiyo pamoja na familia yake, Faizar Kasamia, baada ya kuguswa na hali ya Mama huyo ametoa vitu vya aina mbali mbali vyenye thamani ya Shilingi Laki tatu.

Vitu alivyotoa ni pamoja na Nguo,Maziwa (Lactogen), Mafuta, Sabuni na Nepi.

  Na Mbeya yetu

1 comment:

Anonymous said...

Mungu awabarik na awazidishie wote waloguswa kumsaidia huyu dada, MESHACK MWAKILEMBE pande za ilombe apa, be blessed mr. bloger