Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, November 28, 2013

PSPF YAANZISHA MAFAO MAPYA KWA WATU WOTE

 Amina Mtingwa, Afisa Mwendeshaji wa mfuko wa PSPF kutoka Makao makuu akisalimiana na 
Waziri wa Uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe alipotembelea banda la PSPF
 Amina Mtingwa, Afisa Mwendeshaji wa mfuko wa PSPF kutoka Makao makuu akiongea na wananchi waliotembelea banda hilo




WATANZANIA wametakiwa kujitokeza kwa wingi kujiunga katika  Mifuko ya kijamii hususani Mfuko wa Pensheni wa PSPF Kutokana na maboresho na huduma zake zinazolenga kuwanufaisha wananchi wa ngazi zote.

Mwito huo umetolewa na Afisa Uendeshaji wa PSPF Makao makuu Dar Es Salaam, Murua Kihore katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hizi katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya ukumbi wa mikutano wa Mkapa uliopo Sokomatola Jijini Mbeya.

Kihore amesema lengo la PSPF kuwepo katika maonesho hayo ni kutoa Elimu kwa Wananchi wote bila kujali itikadi, utaifa wala dini kuhusu mafao mapya yalioanzishwa na mfuko huo ambayo yamelenga watu wa ngazi zote kama watumishi wa umma, wafanyabiashara na wajasiliamali wenye uwezo wa kuchangia mfuko kwa hiari.

Amesema mafao mapya yalioanzishwa kwa watu wote ni pamoja na mafao ya elimu, Ujasiliamali, mafao ya uzeeni, mafao ya kifo, mafao ya kujitoa, mafao ya ugonjwa na mafao ya ulemavu.

Ameongeza kuwa kutokana na sheria na sheria mpya ya mifuko ya kijamii inayotaka kila mwananchi kupata fursa sawa katika hifadhi za kijamii, ndiyo maana PSPF imejikita katika kutoa elimu kwa wananchi kujiunga na mfuko huo kutokana na faida watakazo zipata baada ya kuwa wanachama.

Amesema hivi sasa PSPF iko kwenye mkakati wa kubadilisha majina yake kutoka kuwa mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umma na kuwa mfuko kwa kila mtu kutokana na baadhi ya watu kuamini kuwa mfuko huo upo kwa ajili ya watumishi wa umma tu.

Kwa upande wake Amina Mtingwa, Afisa Mwendeshaji wa mfuko wa PSPF kutoka Makao makuu amesema mfuko huo unafaida kubwa kwa wajasiliamali wenye vipato vya kawaida kwa sababu zimefunguliwa ofisi Mikoa yote Tanzania Bara na Visiwani ambapo pia mwanachama anaweza kupata taarifa za mfuko popote atakapokuwepo kupitia mitandao pamoja na mafao kufika kwa wakati mteja anapohitaji.

Amezitaja baadhi ya kazi za mfuko kuwa ni pamoja na kusajili wanachama wapya kwenye mfuko, kukusanya michango kutoka kwa wanachama, kufanya uwekezaji katika vitega uchumi vilivyosalama na kulipa mafao kwa wanachama aliyekamilisha taratibu.

Afisa huyo amezitaja baadhi ya njia ambazo mchangiaji anaweza kuchangia mfuko huo kuwa ni pamoja na Tawi la Benki ya NMB Kupitia akaunti namba 20101100085 kwa jina la Public Service Pension, au CRDB kwa jina hilo hilo namba 01J1120380700 na kupitia mitandao ya simu ya Mpesa na Tigo Pesa.

Ameongeza kuwa Mchangiaji huyo anaweza kuchanga kadiri anavyopata ambapo kima cha chini ni Shilingi 10,000 kwa Mwezi ambazo Mtu yoyote anaweza kutoa fedha hizo aidha kwa wiki, mwezi, msimu au kwa Mwaka ili mradi azingatie kima cha chini cha uchangiaji.

Na Mbeya yetu





No comments: