Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, November 28, 2013

HIGHLANDS SEEDS YATAKA WANANCHI WATUMIE MBEGU BORA

Waziri wa Uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe alipotembelea banda la kampuni ya uzalishaji Mbegu Highlands Seeds,
  katika Maonesho ya Kimataifa ya kibiashara yanayofanyika katika viwanja vya ukumbi wa mikutano wa Mkapa uliopo Sokomatola Jijini Mbeya.
 
Meneja masoko wa kampuni ya uzalishaji wa Mbegu ya Highlands Seeds, John Mbele, wa pili kushoto akionge na mwandishi wetu


WAKATI watanzania wengi wakielekea katika msimu wa kilimo, wameshauriwa kuwa makini na wauzaji wa pembejeo za kilimo ili kuepuka kuuziwa mbegu zisizokuwa na ubora na kuingizwa kwenye umaskini.

Rai hiyo imetolewa na Meneja masoko wa kampuni ya uzalishaji wa Mbegu ya Highlands Seeds, John Mbele, katika maonesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea katika viwanja vya ukumbi wa mikutano wa Mkapa uliopo Sokomatola Jijini Mbeya.

Amesema baadhi ya wafanyabiashara siyo waaminifu na kuwauzia wakulima mbegu feki ambazo wakizipanda hazioti au zikiota hushindwa kutoa mazao yenye tija kwa mkulima.

Amesema ili kukabiliana na adha hiyo ni vema wakulima wakawa wanadai risiti baada ya kununua mbegu kutoka kwa muuzaji au wakala ili pindi zinapomletea madhara ili rahisi kumchukulia hatua za kisheria.

Akizungumzia Mbegu wanazoshughulika nazo za Mtama, Alizeti, Ufuta, Mtama na mahindi kuwa ni mkombozi kwa mkulima kutokana na kufanyiwa utafiti na kuzalishwa hapahapa nchini kwa kuzingatia mahitaji ya Watanzania.

Amesema mbegu za kutoka Highlands Seeds zinastahimili magonjwa, ukame pamoja na kutokuwa na pumba nyingi kuliko unga jambo ambalo ni mkombozi kwa mkulima na mwanachi wa kawaida kwa sababu ya kumwingizia kipato.

Meneja huyo ameongeza kuwa wapo matapeli wengi wanaotumia majina na nembo za kampuni hiyo kuzalisha mbegu zisizokuwa na ubora kwa lengo la kuharibu biashara na kuwarudisha nyuma wananchi kimaendeleo na mapato kwa ujumla.

Amesema ili kuepuka adha hiyo wakulima wameshauriwa wanaponunua mbegu kuhakikisha wanadai risiti na kutotupa mifuko waliyonunulia ili iwe rahisi kuwabana wauzaji matapeli.

Mwisho.

Na Mbeya yetu


No comments: