Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, April 26, 2013

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewataka wananchi nchini kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mamlaka hiyo katika kutekeleza hatua za uhamaji wa urushaji wa matangazo kutoka Analojia kwenda Digitali.

Afisa Uhusiano wa Tcra Innocent Mungi wakati akizungumza na Vyombo vya Habari vya Mkoa wa Mbeya katika Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Mkapa, kuhusu zoezi la uzimaji wa Mitambo ya Analojia katika Mkoa wa Mbeya.

Baadhi ya waandishi wa habari wa mkoa wa Mbeya wakiwa makini kusikiliza
Kizazi cha Digitali



MAMLAKA  ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewataka wananchi nchini kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mamlaka hiyo katika kutekeleza hatua za uhamaji wa urushaji wa matangazo kutoka Analojia kwenda Digitali.
  
Mwito huo ulitolewa na Afisa Uhusiano wa Tcra Innocent Mungi wakati akizungumza na Vyombo vya Habari vya Mkoa wa Mbeya katika Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Mkapa, kuhusu zoezi la uzimaji wa Mitambo ya Analojia katika Mkoa wa Mbeya.
  
Mungi alisema zoezi la uzimaji wa mitambo ya utangazaji wa Televisheni ya mfumo wa Anaolojia ulianza kutekelezwa Disemba 31, Mwaka jana katika Jiji la Dar Es Salaam kutokana na makubaliano ya nchi wanachama wa  Jumuiya ya Afrika Mashariki.
  
Alisema wananchi wanapaswa kutoa ushirikiano kwao kutokana maandalizi ya kuzima mitambo hiyo katika Jiji la Mbeya kukamilika kwa kuwashirikisha wananchi wa Vitongoji vyote ambapo mitambo hiyo itazimwa rasmi Saa sita Usiku Aprili 30, Mwaka huu.
  
Afisa huyo alisema Elimu kwa umma kupitia mbinu mbalimbali kuhusu mchakato wa kuhamia katika Teknolojia ya mfumo wa Utangazaji wa Digitali imekuwa ikitolewa kwa kiwango cha kuridhisha.
  
Alisema matangazo ya Digitali ni mazuri kwa sababu huwafikia watazamaji wengi zaidi kuliko Mfumo wa Analijia ambapo kati ya Watazamaji wanaofikia asilimia 24 ni Asilimia 22 wanaofikiwa na matangazo hayo.
  
Kwa upande wake Mhandisi wa Maswala ya utangazaji kutoka Mamlaka ya mawasiliano, Andrew Kisaka alisema katika Awamu ya kwanza ya uzimaji wa mitambo hiyo itaishia katika Mkoa wa Mbeya.
  
Alisema hatua ya awamu ya pili itatangazwa baadaye ambapo aliitaja mikoa ambayo imezimwa katika awamu ya kwanza kuwa ni Dar Es Salaa (31/12/2012), Dodoma na Tanga(31/1/2013), Mwanza(28/2/2013), Moshi na Arusha  (31/3/2013) na Mbeya ambayo itazimwa mwishoni mwa mwezi huu.
  
Aliongeza kuwa baadhi ya vigezi ambavyo viliwekwa na Serikali kabla ya kuanza kutekeleza suala hilo ni pamoja na Kuhakikisha kuwa eneo linalozimwa lina huduma ya matangazo ya Digitali, Elimu kwa umma itolewe kuhusu zoezi la uzimaji kabla ya utekelezaji.

Alivitaja vigezo vingine kuwa ni Kuendelea kuonekana kwa Chaneli tano za Bure ambazo ni Tbc, Star Tv, Itv, Eatv na Capital Televisheni, Uwepo wa Ving’amuzi vya kutosha katika eneo husika pamoja na kupunguza makali ya bei.




No comments: