Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, February 28, 2013

SERIKALI wilayani Rungwe imeendelea kuwashukuru wadau wa elimu kuendelea kutoa misaada mbalimbali ili kuweza kumalizia ujenzi wa vyumba vya madasara katika shule za wilayani Rungwe mkoani Mbeya

Mkuu wa wilaya ya Rungwe, Chrispin Meela, akiokea msaada wa mifuko ya saruji toka kwa meneja wa kampuni ya Melt George mwamakula 
Mkuu wa wilaya ya Rungwe, Chrispin Meela, akiishukuru kampuni hiyo kwa msaada waliotoa kwa wilaya yake ya Rungwe


SERIKALI wilayani Rungwe imeendelea kuwashukuru wadau wa elimu kuendelea kutoa misaada mbalimbali  ili kuweza kumalizia ujenzi wa vyumba vya madasara katika shule za wilayani hapo na kuhakikisha wanafunzi wote waliofaulu mitihani yao ya darasa la saba mwaka jana kujiunga na kidato cha
kwanza haraka iwezekanavyo.

Kauli hiyo ya Serikali imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Rungwe, Chrispin Meela, mara baada ya kupokea  msaada wa mifuko 200 ya Saruji yenye thamani ya zaidi ya shilingi 3.5 Milioni, kutoka kwa kampuni ya Mohamed Enterprises Limited (Metl) yenye kiwanda cha kusindika majani ya Chai wilani hapo amabyo   alikabidhiwa jana wakati alipotembelea kiwanda hicho kwa lengo la kujionea uzalishaji wake.

Meela alisema kuwa moja ya matunda ya wawekezaji ndani ya wilaya hiyo ni kuona namana wanavyokuwa mstari wa mbele katika kuisadia jamii inayowazunguka na si vinginevyo na kwamba hilo lipo hata katika shueria za uwekezaji nchini.

Alisema kuwa juhudi zinazooneshwa na wawekezaji wa ndani katika kuhakikisha watoto wote waliofaulu mitihani yao ni kuendelea kujenga na kukarabati vyumba vya madarasa.

Mkuu huyo alibainisha kwamba misaada hiyo imekuja kwa muda mwafaka kwasababu zaidi ya wanafunzi 700 waliofaulu mtihani wao wa darasa la saba mwaka jana wameshindwa kujiunga na kidato cha kwanza wilayani hapo kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa hivyo misaada hiyo itasaidia kukamilisha ukarabati huo na kuona wanafunzi wote wanakwenda shule.

“Niendelee tu kuwashukuru watu muhimu kama hawa wa Kampuni ya Mohamed Enterprises kuliona kuwa wilaya yetu tunawanafunzi zaidi ya 700 walioshindwa kujiunga na kidato cha kwanza kutokana na upungufu wa vyumba vya madarasa,”alisema na kuongeza.

“Tunatambua kuwa licha ya mikakati ya serikali ya kuhakikisha hadi kufikia mwishoni mwa mwezi wa tatu  ukarabati wa vyumba hivyo uwe umekamilika na wanafunzi wawe wameanza masomo, makampuni ya viwanda vilivyo wilayani hapa vimejitoa kweli kutusaidia kwa mwezi uliopita tu tumepokea mifuko 100 ya saruji  kutoka kampuni moja na nyinyi leo mnatuunga mkono kwa kutupatiwa mifuko 200 mingine kweli msaada mkubwa sana kwetu,” alisema Meela.

Awali Meneja wa Kamupni hiyo ya Metl, George Mwamakula, alisema kuwa wao kama wawekezaji wa ndani moja ya furaha yao kuona wanaishi na jamii ya watu waliosoma hivyo hawataona kazi kuendelea kusaidia jamii hiyo katika sekta ya elimu pamoja na sekta nyingine muhimu kama vile maji, umeme, afya na barabara.

“Hata sisi tunatambua wazi kwamba jamii isiyokuwa na elimu ya kutosha wawekezaji hawawezi kukaa kwa amani kwani migogoro isiyokuwa lazima lazima itatokea tu lakini kama jamii hii itapatiwa elimu ya kutosha hakutakuwa na migogoro baina ya wawekezaji na wananchi husika kwani mgogoro wowote unajipotokeza inakuw rahisi kuutatua kwa amani zaidi,” alisema Mwamakula.

No comments: