Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, December 4, 2012

WAANDISHI WA HABARI MBEYA KUSHIRIKI USAFI MBALIZI

 KUSHOTO NI MWAKILISHI WA MKURUGENZI WA WILAYA YA MBEYA EMMANUEL MWAIGUGU AMBAYE NI MRATIBU WA KITENGO CHA KINGA NA TIBA AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA BAADHI YA VIJANA WA MBALIZI LEO BAADA YA KIKAO CHA PAMOJA KILICHOFANYIKA UKUMBI WA HOTEL YA NSUNGWE.
Standi kuu ya mbalizi

BAADHI ya waandishi wa habari mkoani Mbeya wamesema kuwa watahusika kwa asilimia 100 katika kuungana na vijana wa Mji mdogo wa Mbalizi wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani humo kufanya usafi wa kufagia na kuzibua mitaro unaotarajia kufanyika kesho (Jumatano).

Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa Nsungwe uliopo Mbaizi, mratibu wa Vijana wazalendo wa mji wa Mbalizi Gordon Kalulunga, alisema kuwa baadhi ya waandishi wa vyombo mbalimbali waliopo mkoani Mbeya wamefurahishwa na wazo la vijana hao hivyo wamemwakikishia kuwa nao wataungana nao.

Kalulunga alisema kuwa baadhi ya waandishi hao wanatoka kwenye Mgazeti ya Tanzania Daima, Mwananchi, Sauti huru, Jambo Leo na Habari leo, Televisheni ya Taifa TBC1, Star TV na redio  Mbeya yetu blog zilizopo mkoani Mbeya.

Alisema anawashukuru waandishi hao na wanataaluma wengine ambao watashiriki katika tukio hilo la kihistoria na kwamba vijana wa Mbalizi wanaomba kupitia kwao vijana wengine poote Tanzania wafanye hivyo katika maeneo yao ili kuifanya Tanzania salama.


‘’Mbali na waandishi wa habari na vijana wengine ambao watatoka nje ya wilaya yetu ya Mbeya Vijijini, tumekutana na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa wilaya yetu Emmanuel Mwaigugu ambaye ni mratibu wa kitengo cha kinga na tiba ameonyesha jinsi gani Serikali imethamini wazo hili na kuwa tayari kushirikiana nasi pale tunapokwama’’ alisema Kalulunga.

Sanjari na hayo alisema baada ya kufanya usafi huo katika eneo la Tarafani watafanya tathimini na kujiwekea malengo ya kufanya usafi kama huo katika eneo linguine.

Naye Kijana Raphael Kajange alisema kuwa hapo baadae anaamini kila mwananchi atakuwa balozi wa kulinda na kutunza mazingira ya mji wa Mbalizi na kila kaya.


No comments: