Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, December 5, 2012

VIJANA WA MJI MDOGO MBALIZI MBEYA WILAYANI MBEYA VIJIJINI WAFANYA USAFI WA KUZIBUA MIFEREJI NA KUTENGENEZA BARABARA

Vijana wa Mji mdogo wa Mbalizi wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani Mbeya leo wamefanya kazi ya kufagia kuzibua mifereji na kutengeneza barabara kivutio kikubwa kilikuwa kwa kina dada kwani walijitokeza kwa wingi na kuchapa kazi sambamba na kaka zao
Hakika vijana wa Mbalizi tuwape pongezi kwa kazi nzuri wanayoifanya kwani ni vijana wachache sana wanaojitolea kufanya kazi hizo za usafi wa kujitolea

Vijana hao wa mbalizi wamesema si vema kila kitu kuiachia serikali waka kazi nyingine tunaweza fanya kama hizi za usafi na kutunza mazingira hapa vijana wakipeana mikakati ya kuboreza mjiwao wa mblizi kwa usafi
Hakika ina pendeza mweshimiwa diwani kata ya utengule usongwe ambae pia ni mwenyekiti wa kijiji cha Mbalizi mwenye koti la kijani Mh. Eliah Mkono na mkuu wa kitengo cha kinga na tiba Mbeya vijijini  Emanuel Mwaigugu wakifurahia baada ya kuona vijana wamejitokoza kwa wingi kusafisha mji wao wa mbalizi
Mweshimiwa diwani akikagua kazi inayoendelea ya kuzibua mifereji na kutengeneza barabara
kazi inaendelea

Mweshimiwa diwani hakuwa nyumba katika kuwasaidia vijana 
Kwenye kazi utani pia upo ili kazi iende vizuri dada na kaka wanataniana
Safi sana vijana wa Mbalizi
Mratibu wa Vijana wazalendo wa mji wa Mbalizi Gordon Kalulunga,akiwa na kiongozi mwenzake wakifurahia jinsi kazi inavyoendelea
Hali halisi ya mifereji ya mbalizi ni hii sasa vijana ndiyo wanaizibua
Baada ya kuzibuliwa  kwa ujumla mbeya yetu tunawapongeza sana vijana wa mbalizi kwa umoja wenu tunaomba na vijana wengine muige mfano huo wa kujitolea kufanya usafi zoezi la usafi litaendelea kesho

picha na Mbeya yetu

No comments: