Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, May 23, 2012

KAMPENI ZA UCHAGUZI CHUO KIKUU CHA TEOFILO KISANJI (TEKU) ZAZINDULIWA RASMI.





Habari na Ezekiel Kamanga.
Wanawake wawili wajitokeza kugombea nafasi ya Urais na Makamu Rais.

Kampeni za uchaguzi wa 
kumpata Rais wa Chuo kikuu cha Teku, zimezinduliwa rasmi jana katika 
ukumbi wa Mwasakafyuka huku wagombea wakinadi sera zao.




Kampeni hizo zilizinduliwa
na Dakta Mozes D, na kusimamiwa na mkufunzi wa chuo Bwana Alawi 
Mikidadi ambapo Mkurugenzi wa uchaguzi Bi Nyemba Joyce aliweka hadharani
wagombea watakao wania viti vya urais na makamu rais.




Majina hayo upande wa rais
ni Bi Somi Irene, Bwana George Godbless na Joshua Jason na upande wa 
Makamu ni Bi Wilson Gwantwa, Bwana Yohanna Yesse na Deus Petro.


Mwenyekiti wa tume ya 
uchaguzi Bwana Kavenga Emmanuel amesema kwamba mchakato wa uchaguzi 
ulianza Mei 9 mwaka ahuu kwa kujaza fomu ambapo wanachuo 70 walijitokeza
kuomba nafasi mbalimbali.




Aidha Mei
19 na 20 wagombea walifanyiwa wagombea usaili na kwamba majina 
yaliyotajwa hapo juu ndio yaliyopitishwa na tume hiyo na kwamba kampeni 
zimeanza rasmi jana ambazo zitaendelea mpaka Mei 28 asubuhi na uchaguzi 
utafanyika Mei 29 mwaka huu na matokeo yatatangazwa mei 30 mwaka huu na 
viongozi wote Rais na baraza la mawaziri kuapishwa Juni mosi mwaka huu.




Mwenyekiti huyo Bwana 
Kavenga amewataka viongozi hao kufanya kampeni za amani bila matusi 
kwani kampeni kwa kufanya hivyo haitawasaidia kupata kura, bali 
itawashushua heshima zao.


Kwa upande wake Rais 
anayemaliza muda wake Bwana Ambukege Imani ameishukuru tume ya uchaguzi 
kwa mchakato mzima na anafurahi kumaliza muda wake chuo kikiwa na amani 
na kuwataka watakaopata nafasi za kuongoza wazingatie sheria, demokrasia
na upendo ili kuleta mshikamano katika chuo, ili wanaoongozwa wajisikie
kuwa na amani kuwepo chuoni hapo badala ya kutatua migogoro isiyokuwa 
na maana.

Baadhi ya wabunge walipita bila kupingwa, kutokana na baadhi ya maeneo waliyokuwa wakiyagombea kutokuwa na wapinzani.


Hata
hivyo kujitokeza kwa wanawake kumeleta msisimko wa uchaguzi huo huku 
wanawake wakitoa majigambo kuwa wanawake wanaweza hata pasipo kuwezeshwa
na kwamba chuo hicho hakijawahi kupata viongozi wa juu ambao ni 
wanawake na kwamba imefika zamu yao kuongoza.

No comments: