Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Saturday, January 7, 2012

ASILIMIA 70 YA UHALIFU MBEYA YADHIBITIWA



Mkuu wa upelelezi mkoa wa Mbeya Anacret Malindisa aliyehamishiwa Jijini Dar Es Salaa


ASILIMIA 70 za uhalifu na maovu mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea mkoani Mbeya yamedhibitiwa kutokana na jitihada za ushirikiano kati ya Jeshi la polisi na wadau wakiwemo wazee na viongozi wa mila.

Hayo yalielezwa juzi na  aliyekuwa Mkuu wa upelelezi mkoa wa Mbeya Anacret Malindisa aliyehamishiwa Jijini Dar Es Salaa kikazi, katika hafla fupi ya kumuaga iliyoandaliwa na Muungano wa jamii Tanzania(MUJATA).


Alisema Viongozi hao wa mila, kwa kiwango kikubwa wamesaidia kuwafichua waharifu ambao walikuwa wakifanya maovu katika jamii.

Alisema ushirikiano alioupata kutoka kwa machifu na wazee mbalimbali akiwa madarakani ulimsaidia kwa kiasi kikubwa kupambana na vitendo vya mauaji yakiwemo uchunaji ngozi,ujambazi na kilimo cha bangi kwa baadhi ya maeneo ndani ya mkoa na kuufanya mkoa wa mbeya kuwa shwari.

Mwenyekiti wa Muungano wa Jamii (MUJATA) Shayo Soja alisema kuwa baada ya kuundwa na kusajiliwa kwa  umoja huo mwaka  2009 kumekuwa na mafakio mengi ya kupambana na  maovu mbalimbali katika jamii kutokana na ushirikiano mkubwa uliopo kati ya wazee,jamii,machifu na wataalam wa jadi .

Alisema mbali na wadau hao, ushirikiano mzuri uliopo kati ya MUJATA na jeshi la polisi umefanikisha kukomesha maovu mengi yaliyokuwa tishio la amani kwa wageni waliokuwa wakitembelea mkoa wa Mbeya pamoja na wenyeji.

“Tumejitahidi kuibua maovu mbalimbali ambayo mengi yalishindikana kwa njia ya kawaida hivyo kutokana na  kila kundi wakiwemo wazee,machifu na watalaam  wa jadi kushiriki vyema katika kuwafichua waharifu katika maeneo yao tumefanikisha kwa kiasi kikubwa na ndiyo maana amani ipo mkoani Mbeya,” alisema Chifu Soja.

Hata hivyo aliwatupia lawama baadhi ya viongozi kwa kutoungana nao katika kampeni hizo hususani viongozi wa siasa akiwemo Mbunge wa Jimbo la Mbeya mjini Joseph Mbilinyi (CHADEMA) na mbunge wa jimbo la Mbeya vijijini Mch.Lackson Mwanjale (CCM).

Alisema wabunge hao wameshindwa kujenga ushirikiano wa karibu na umoja huo katika mapambano dhidi ya matendo maovu katika jamii ili hali wao ni wawakilishi wa wananchi.

Kwa upande wake  Mkuu wa upelelezi  Mkoa Mbeya aliyehamia na kubadili nafasi ya Malindisa, Mwita Chacha ameahidi kushirikiana na uongozi wa MUJATA katika mapambano dhidi ya matendo maovu ndani ya jamii.

Alitoa wito kwa  wazee,machifu na wataalam wa jadi kote nchini kujiunga na chama hicho kwa lengo la kufanikisha mapambano  dhidi ya maovu katika jamii ili wafanye kazi nchi nzima.

No comments: