Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, November 22, 2011

RC- MBEYA HALMASHAURI HAKIKISHENI MMEPIMA MAENEO YOTE MLIYOYATENGA KWA AJILI YA UWEKEZAJI‏

 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro wakati wa ufunguzi wa mkutano wa baraza la biashara la Mkoa wa Mbeya.
Wakuu wa wilaya wakimsikiliza Mkuu wa mkoa Mbeya
Baadhi ya wawekezaji wakiwa makini kumsikiliza mkuu wa mkoa Mbeya
Wafanya biashara wa jiji la mbeya 
Wakurugenzi wa halmashauri za mkoa wa mbeya wakiwafuatilia kwa makini hotuba ya mkuu wa mkoa Mbeya
Wadau mbalimbali walikuwepo



HALMASHAURI za  Mkoa wa  Mbeya, zimetakiwa  kutenga  maeneo yaliyopimwa  kwa ajili ya uwekezaji ili kuepuka migogoro baina  ya wananchi na wawekezaji ambayo imekuwa ikirudisha nyuma maendeleo.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro wakati wa ufunguzi wa mkutano wa baraza la biashara la Mkoa wa Mbeya.

Alisema, ni vema halmashauri hizo zikatenga maeneo ya ardhi ambayo tayari wameshayapima kwa ajili ya uwekezaji  na si kuwatumbukiza wawekezaji kwenye migogoro na wananchi.

“Halmashauri  zinapaswa kuyapima maeneo ambayo yametengwa kwa ajili ya uwekezaji ili kuwaokoa wawekezaji na migogoro ya wananchi ambayo hupoteza muda kwa kupelekana mahakamani,

Alisema, pia halmashauri hizo zinatakiwa kusghulikia matatizo ya wananchi  kama vile kulipa fidia kwa wale  watakaoitajika kuondoka kwenye maeneo yao kwa ajili ya uwekezaji.

“Halmashauri zinapaswa kufahamu kuwa zinawajibu wa kushughulikia matatizo ya wananchi kama vile kulipa fidia kwa watakaotakiwa kuondoka na si kuwaachia matatizo wawekezaji na ambao huishia kupelekana mahakani,

Aidha, Mkuu huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Balaza hilo aliwataka watendaji wa serikali na wanasiasa kwa ujumla  kuacha kupoteza muda kwa kujadili mambo ambayo hayana msingi bali watumie muda huo kujikita kwenye shughuli za maendeleo.

“Tusipoteze muda kuzungumzia mambo ambayo hayana msingi bali tutumie muda huo kuzungumzia mambo ya maendeleo ambayo ndio msingi wa Taifa katika kuleta maendeleo,

No comments: