Chama
 cha Wamiliki/Waendeshaji wa Mitandao ya Jamii nchini 'Tanzania Bloggers
 Network' – TBN inawaomba wanachama wake wote kutotumia taarifa ama 
habari au picha yoyote kutoka katika mkutano wa maadhimisho ya Uhuru wa 
Vyombo vya Habari (WPFD) unaofanyika kitaifa mkoani Mwanza. 
Kamati
 Kuu ya Uongozi TBN imefikia hatua hiyo leo baada ya kujadiliana na 
kujiridhisha kuwa kumekuwepo na taasisi za tasnia ya habari ambazo 
zimekuwa zikiwatenga wanahabari wa mitandao ya kijamii (bloggers) na 
kutotambua umuhimu wao wakati sehemu kubwa ya taarifa mbalimbali nchini 
husambazwa na mitandao hiyo.
TBN
 iliyosajiliwa rasmi serikalini Aprili 2015 na kupewa namba ya usajili; 
S. A 20008 inawataka wanachama wake kutotoa ushirikiano wa sina yoyote 
kwa taasisi ambazo zinawatenga bloggers. 
Tunasikitika
 kufikia hatua hii ila hamna jinsi. TBN itasikitika na kumshangaa 
mwanachama wake au blogger asiye mwanachama kutounga mkono agizo hili, 
na kwenda kinyume na agizo hili. Muda umefika ‘Bloggers’ kudai heshima, 
kutambulika na kuthaminika kama tasnia ya habari ingine yoyote.
Imetolewa na;- 
Mwenyekiti wa Muda wa TBN
Joachim E. Mushi
03/05/2016

No comments:
Post a Comment