Mkuu wa Wilaya ya Karonga nchini Malawi,Rosemary Moyo(aliyesimama) akizungumza jambo katika kikao cha ujirani mwema huku Mkuu wa Wilaya ya Kyela Dk.Thea Ntara akimsikiliza kwa makini. |
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha ujirani mwema kati ya Wilaya ya Karonga na Wilaya ya Kyela wakifuatilia mjadala unaoendelea |
ILI
kuimarisha ujirani mwema kati ya Wilaya ya Kyela na Karonga ya Nchi jirani ya
Malawi, Wilaya hizo zimekutana katika kikao cha pamoja ili kujadili changamoto
zinazowakabili.
Kikao hicho
cha ujirani mwema kilifanyika juzi katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya
Kyela kwa ajili ya kujadili changamoto zinazozikabili Wilaya hizo.
Katika kikao
hicho ambacho kilihudhuriwa na Mkuu wa Wilaya
ya Kyela Dk. Thea Ntara aliyewakilisha upande wa Tanzania na kwa upande wa
Wilaya ya Karonga iliwakilishwa na Rosemary Moyo ambapo baadhi ya changamoto
kubwa zinazozikabili Wilaya hizo na kujadiliwa kuwa ni pamoja na wahamiaji
haramu,madawa ya kulevya,pombe kali na wizi wa pikipiki.
Wakizungumza
katika kikao hicho, Baadhi ya wajumbe kutoka pande zote mbili walisema tatizo la wahamiaji haramu kutoka nchi za
Ethiopia,Somalia,Congo,Burundi,Rwanda na Nigeria kunachangiwa na ukosefu wa
umakini kutoka mipaka ya kaskazini ambapo huwaacha wahamiaji hao kuingia
kiholela.
Walisema
sababu nyingine inachangiwa na baadhi ya watumishi wa umma wa pande hizo
mbili kutodhibiti vitendo hivyo kutokana wa baadhi
ya wahamiaji kutumia pesa pindi wanapokamatwa na baadhi ya maafisa usalama
wasio waaminifu.
Kwa
upande wake Mkuu wa Wilaya ya Karonga, Rosemary Moyo alisema kuwa Watanzania na
Wamalawi ni ndugu wa damu ambao wametenganishwa na wakoloni kwa njia ya mpaka
wa mto Songwe kwani mpaka sasa raia wa mpakani huvuka kutembeleana kila siku na
wengi wao wameoleana kutoka pande hizo mbili.
Alisema
kutokana na tatizo hilo kubwa kwa nchi
hizo Serkali zote huingia gharama kubwa kuwatunza na kuwasafirisha wahamiaji
haramu kuwarejesha nchi walizotoka.
Kwa
upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kyela Dk. Thea Ntara alisema Wilaya ya Kyela
imeimarisha ulinzi mpakani kwa kushirikiana na wananchi ndiyo maana
wamefanikiwa kukamata wahamiaji wengi haramu waliojaribu kuvuka mpaka kupitia
wilaya hiyo hivyo juhudi kubwa zifanyike ili kuhakikisha tatizo hilo
linakomeshwa kabisa.
Aliongeza
kuwa elimu itolewe kwa raia wa pande
zote mbili ili watu wanaowatilia shaka watolewe taarifa katika vyombo vya
ulinzi na usalama vya nchi hizo mbili.
No comments:
Post a Comment