Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, September 30, 2015

WACHUNGAJI WA MORAVIANI JIMBO LA KUSINI MAGHARIBI WATIMULIWA KWENYE NYUMBA ZA KANISA

 Kibao kikionesha makao makuu ya Kanisa la Moraviani Jimbo la Kusini Magharibi
Geti la Kanisa likiwa limefungwa kufuatia mgogoro wa Kanisa hilo uliokuwepo awali na kupelekea baadhi ya wachungaji kusimamishwa

  
Baraza la Nyumba na Ardhi  Wilaya ya Mbeya limewaondoa katika nyumba za Kanisa Wachungaji watano waliokuwa  Watumishi katika Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi.

Amri hiyo imetolewa katika Baraza la Wilaya na Mwenyekiti wake Crispin Hatson, katika kesi namba 146 b ya mwaka 2014 iliyofunguliwa na Kanisa baada ya Wachungaji hao watano kufukuzwa kazi lakini walikataa kuondoka katika nyumba za Kanisa.

Walioondolewa katika nyumba za Kanisa ni pamoja na aliyekuwa Mwenyekiti wa Kanisa hilo Nosigwe Buya aliyekuwa akiishi Jacaranda,Jamson Mwiligumo aliyekuwa akiishi Meta,Edward Chilale aliyekuwa akiishi Ushirika wa Bethelehemu Mama John,Nehemia Mwalupembe aliyekuwa Ushirika wa Panda Hill Songwe na Joseph Mwakyoma aliyekuwa akiishi Itiji Jijini Mbeya.

Mweyekiti wa Baraza la Ardhi amesema kuwa maamuzi hayo ni madogo katika shauri mama linalosikilizwa katika Baraza hilo shauri ambalo lilifikishwa mapema mwaka jana na Kanisa likiwataka wahame baada ya kuwaachisha kazi.

Aidha Mwenyekiti wa Baraza amesema shauri mama litaendelea kusikizwa Barazani hapo Novemba 11 mwaka huu na kwamba kwa sasa Wachungaji hao hawapaswi kuwepo katika nyumba za Kanisa wakati shauri likiendelea kusikilizwa.

Mgogoro huo wa Kanisa umedumu kwa zaidi ya miaka miwili ambapo Wachungaji hao wamekuwa na Mgogoro na Mwajiri wao ambaye ni Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi.

Baadhi ya madai ni pamoja na kupinga kuenguliwa Uenyekiti Mchungaji  Nosigwe Buya na kutaka kuitishwa kwa Sinodi ya dharula ili kumrejesha kazini Mwenyekiti huyo baada ya tuhuma za ubadhilifu wa fedha za Kanisa.

No comments: