Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, August 18, 2015

PINDA AFUNGA MAFUNZO YA UONGOZI DARAJA LA KWANZA MAGEREZA KIWIRA MBEYA.

Waziri MkuuPinda akitoa hotuba ya kufunga mafunzo ya uongozi daraja la kwanza.
   Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiwa amesimama imara kupokea salam maalumu kutoka kwa askari wa magereza wakati wa mahafali ya kuhitimu mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi ya 21.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akitoa heshima wakati wa mahafali ya kuhitimu mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi ya 21.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akikagua gwaride la askari wa magereza wakati wa mahafali ya kuhitimu mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi ya 21.
Kiongozi wa Gwaride akitoa maelekezo kwa askari.
 Waziri Mkuu Mizengo Pinda akimtunuku cheo cha Ukoplo mmoja wa wahitimu kwa niaba ya wenzie wakati wa mahafali ya kuhitimu mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi ya 21.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akitoa Cheti kwa mwanafunzi aliyefanya vizuri wakati wa mahafali ya kuhitimu mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi ya 21.
  Kikosi cha Bendera kikipita mbele ya mgeni rasmi.

Gwaride likipita mbele ya mgeni rasmi kwa mwendo wa pole na kasi.
Waziri Mkuu akipita kukagua gwaride maalum.
Wahitimu wa mafunzo ya uongozi wakionesha umahiri wao wa ukakamavu kwa kuvunja vitu vigumu.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa meza kuu.
Brass band ya Magereza ikitumbuiza.
Wahitimu wakiwa kwenye gwaride maalum.
Watoto wadogo wakiwaimbia wahitimu wimbo wa kuwaaga.
Mkuu wa Chuo cha Magereza Kiwira, Tranford Mtilindula akisoma risala ya Chuo kwa mgeni rasmi.
Wahitimu wakiimba wimbo maalum katik mahafali yao.
Kamishna wa Magereza John Minja akimkaribisha mgeni rasmi kutoa hotuba na kufunga rasmi mafunzo.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Mbarak Abdulwakil akitoa salamu za Serikali.
Wahitimu wakiwa katika ukumbi wa mikutano.
Waziri mkuu akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya ulinzi na usala Mkoa wa Mbeya.
 Baadhi ya wananchi waliojitokeza kushuhudia mahafali ya wahitimu wa mafunzo ya uongozi daraja la kwanza.

WAZIRI Mkuu Mizerngo Pinda amefunga mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kwa Maaskari Magereza kozi namba 21 Kiwira Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya.
Akifunga mafunzo hayo pamoja na kuwatunuku vyeo vya Ukoplo wa Magereza Waziri Mkuu aliwataka Maaskari Magereza kuzingatia nidhamu katika kazi kuwa na uadilifu pamoja na kuzingatia haki za binadamu na utawala bora wakiwa kazini.
Alisema Askari yeyote anapaswa awe na nidhamu ya hali ya juu katika utekelezaji wa majukumu yake kwa kufanya kazi kwa uadilifu na kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni jambo litakalotoa mfano kwa askari wa ngazi za chini.
Alisema Tanzania imeridhia na kusaini mikataba mbali mbali ya kimataifa kama mwanachama wa Umoja wa Mataifa hivyo inapaswa kutekeleza kanuni hizo kwa kuhakikisha wafungwa wanahudumiwa kwa kuzingatia misingi ya haki za binadamu.
Waziri Mkuu Pinda alilipongeza Jeshi la Magereza nchini na kwamba ni mfano wa kuigwa katika baadhi ya Nchi kutokana na kufanikiwa katika kipengele chja kuwarekebisha wafungwa na hatimaye kuwa watu wema na kuacha uhalifu.
Alisema jukumu kubwa la Jeshi la Magereza ni kurekebisha tabia za Wafungwawalioko magerezani jambo ambalo hutekelezwa kwa kuwapatia ujuzi na stadi mbali mbali za kuwawezesha kupata ajira  halali wamalizapo vifungo vyao sambamba na kuwapa ushauri nasaha wa kijamii, kisaikolojia na kiroho kulingana na aina ya makosa.
Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Magereza Kiwira, Tranford Ntilindula, alisema mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi ya 21 yalianza juni 1, mwaka huu yakiwahusisha wanafunzi 713 lakini waliuofanikiwa kuhitimu ni 711.
Alisema kati yao ni wanaume 625 na wanawake 86 ambao walipatiwa mafunzo katika Nyanja za utawala na uendeshaji wa magereza,uongozi na utawala bora, sheria zinazoongoza Jeshi la Magereza, ustawi wa jamii, uraia, afya na mafunzo ya kijeshi pamoja na madhara yatokanayo na Rushwa.
Alisema Wanafunzi hao walionesha nidhamu ya hali ya juu na kuzingatia masomo katika muda wote hivyo kustahili kupandishwa vyeo na kuwa Koplo wa Magereza.
Aliongeza kuwa wanafunzi hao walipokuwa masomoni walioonesha moyo wa kujitolea kwa kuchanga fedha taslimu shilingi milioni 1,424,000 kwa ajili ya kununua umeme wa jua(solar power) kwa matumizi ya Zahanati ya Chuo kwa ajili ya kukabiliana na tatizo la kukatika kwa umeme wa Tanesco mara kwa mara.
Naye Kamishna wa Magereza nchini, John Minja alisema Jeshi la Magereza likiwezeshwa linaweza hivyo kuiomba serikali kuipa kipaumbele katika kufanikisha miradi mbali mbali wanayoomba.
Kamishna Minja alimalizia kwa kumuaga Waziri Mkuu Pinda katika utumishi wake Kwa Jeshi la Magereza kumpa zawadi ya Mitamba miwili yenye mimba pamoja na mzinga wa nyuki kwa ajili ya kuendeleza ufugaji pindi akistaafu.

Na Mbeya yetu

No comments: