Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, August 4, 2015

KAMPUNI YA SIMU YA TTCL YAANZISHA HUDUMA YA TELEVISHENI.

  Mkuu wa banda la maonesho la nane nane la TTCL, Amos Gumbo(wa kwanza kushoto)akiwa pamoja na watumishi wa TTCL Mkoa wa Mbeya wakitoa ufafanuzi kwa wateja wao(hawapo pichani) kuhusiana na huduma mpya ya Televisheni.
Afisa wa TTCL ambaye jina lake halikupatikana mara moja akijaribu kuunganisha mitambo katika banda hilo ili kupata chaneli za televisheni bila kutumia king'amuzi.
 Baadhi ya Chaneli za Televisheni zilizopatikana katika zoezi la majaribio ya kutumia internet kupata tv.
Baadhi ya mitambo itakayowawezesha wananchi kupata TV kwa njia ya Internet wakiwa majumbani.
 
KAMPUNI ya simu ya TTCL Mkoa wa Mbeya inawakaribisha wakazi wa mikoa ya Nyanda za juu kutembelea banda la TTCL katika maonesho ya nanenane yanayoendelea katika viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya kujionea huduma mpya.
 
Akizungumza na wananchi waliojitokeza kuangalia huduma katika banda hilo, mkuu wa banda la maonesho la TTCL, Amos Gumbo ambaye pia ni Kaimu Meneja msaidizi wa Biashara Mkoa wa Mbeya alisema huduma mpya walioleta ni IPTV.
 
Gumbo alisema huduma hiyo humuwezesha kila mtanzania kuangalia Televisheni kwa njia ya digitali pasipokuwa na king’amuzi, Ungo wala antenna.
 
Alisema Internet Protocal Television (IPTV) ni rahisi sana pia hulinda usalama wa mwananchi kwani hatakuwa na vitu vya kumshawishi mwizi kumnyemelea kwani atatakiwa kuwa na vitu vichache ili aweze kuangalia Chaneli mbali mbali za Tv.
 
Alivitaja vitu hivyo kuwa ni pamoja na Televisheni ya kawaida, Laini ya simu ya Kampuni ya TTCL,Kompyuta ya aina yoyote na kifurushi hivyo atakuwa na uwezo wa kuunganishiwa huduma hiyo.
 
Aliongeza kuwa huduma hiyo ni nafuu sana na haina vitu vingi vinavyopaswa kuunganishiwa, ambapo mteja atauziwa kwa gharama ndogo ukilinganisha na huduma zingine hivyo wananchi wote mnaombwa kutembelea banda la TTCL kupata maelezo zaidi.
 
NA MBEYA YETU

No comments: