Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Saturday, July 18, 2015

NWAKA MWAKISU ACHUKUA FOMU KUWANIA KUTEULIWA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINI AKIJINADI KUWAUNGANISHA NA KUWAKOMBOA VIJANA.

Nwaka Mwakisu akiwa kwenye ofisi za Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Mbeya mjini tayari kuchukua fomu.
Nwaka Mwakisu akimkabidhi fedha Katibu Msaidizi wa CCM Wilaya ya Mbeya kwa ajili ya fomu za kuwania kuteuliwa kugombea ubunge.

.Mwakisu akisaini daftari maalum baada ya fedha zake kupokelewa.

Mwakisu akikabidhiwa fomu baada ya kukamilisha taratibu zote.
Mwakisu pamoja na mkewe wakitoka kwenye ofisi za Chama baada ya kuchukua fomu.

Nwaka Mwakisu akiwa na viongozi waandamizi wa Wilaya ya Mbeya wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya(mwenye suti katikati), Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mbeya na Katibu wa CCM Wilaya ya Mbeya  baada ya kuchukua fomu.

Nwaka Mwakisu akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu nia yake ya kutaka kuteuliwa kugombea Ubunge.

Baadhi ya waandishi wa habari pamoja na wananchi wakimsikiliza Mwakisu akieleza malengo yake.





MJUMBE wa Mkutano Mkuu(CCM)kupitia Umoja wa Vijana Mkoa wa Mbeya, Nwaka Mwakisu amejitosa na kuchukua fomu ya kuwania kuteuliwa kugombea Ubunge katika Jimbo la Mbeya Mjini(CCM).

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuchukua Fomu hizo, Mwakisu alisema endapo Chama kitampitisha na hatimaye kushinda Ubunge hata kuwa na muda wa kutoa ahadi kwa wananchi wa Jiji la Mbeya bali vitu vingi ameshavifanya kilichobakia ni utekelezaji tu.

Alisema idadi kubwa ya wagombea waliojitokeza asilimia kubwa hawaijui Mbeya pamoja na wakazi wake wanachokihitaji jambo lililopelekea kuwepo kwa vurugu za mara kwa mara kutokana na vijana kutokuwa na Mwakilishi anaewafahamu.

Alisema yeye anajivunia rekodi na mazuri aliyowafanyia vijana na wananchi kwa ujumla wa Jiji la Mbeya yakiwemo ya kuwaunganisha vijana waendesha bodaboda na bajaji ambao tayari wanavyama vilivyosajiliwa na kutambuliwa kisheria.

Alisema kwa upande wa Wanawake na wananchi wengine wakiwomo wafanyabiashara ndogondogo, machinga na watumishi wa umma na mashirika binafsi tayari ameanzisha Benki itakayojulikana kwa jina la Mbeya Youth Microfinance Bank ambayo iko katika hatua za mwisho.

Aliongeza kuwa Benki hiyo itakuwa ya manufaa kwa wananchi wote wa Jiji na Mkoa wa Mbeya ambapo wataweza kupata mikopo nafuu ya fedha pamoja na vitendea kazi huku akitanabaisha kuwa endapo atapata nafasi ya kuwa Mbunge mishahara yake yote itapitia kwenye akaunti ya Benki hiyo.

Mwisho.

No comments: