Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, June 17, 2015

VYAMA VYA UPINZANI VYA KUMBUSHWA WAJIBU WAO.

 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Anderson Kabenga akihutubia mkutano wa hadhara.
 Viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mbeya wakiwa wamekaa meza kuu.
 Mjumbe wa Mkutano mkuu, Mchungaji Jackob Mwakasole akimkabidhi kadi ya chama mwanachama mpya, Benson Mwakilembe.
 Mwanachama mpya, Benson Mwakilembe akipongezwa na Katibu wa CCM Wilaya ya Mbeya.
Baadhi ya wanachama wa CCM wakiwa katika mkutano wa hadhara
 
VYAMA vya upinzani vimetakiwa kujikita zaidi katika kukisoa Chama tawala ikiwa ni pamoja na kueneza sera zinazoweza kuwakomboa wananchi kutoka hapa walipo na kusongambele tofauti na ilivyosasa ambapo wamejikita kupotosha na kueneza chuki.
 
Wito huo ulitolewa  na mjumbe wa mkutano mkuu wa taifa wa CCM kupitia Wilaya ya Mbeya vijijini, Mchungaji Jackob Mwakasole, alipokuwa akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya mahubiri Mbalizi wilayani Mbeya.
 
Mwakasole  alisema mikutano ya vyama vya upinzani imejaa chuki ambazo wanazipandikiza kwa wananchi ili wakichukie Chama tawala bila kuwaeleza ukweli wa mambo mazuri yaliyokwisha fanyika na kueleza sera zao.
 
Alisema lengo la mikutano ni kuwaeleza wananchi juu ya mambo yaliyofanyika ya ukweli lakini wapinzani wanasahau kazi yao ya kukikosoa Chama tawala na badala yake wamekuwa wakitumia nguvu nyingi na mabavu kutaka kuingia madarakani.
 
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mbeya, Anderson Kabange alisema Halmashauri imepata hati safi kwa miaka mitano mfululizo kutoka kwa mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali(CAG) na ndiyo maana miradi mipya inaletwa.
 
Alisema wapinzani wanasema Serikali imechakachua ujenzi wa barabara za lami katika mji mdogo wa Mbalizi lakini wameshindwa kutoa takwimu sahihi juu ya fedha zilizotolewa na kiwango cha barabara kilichojengwa kutokana na kushindwa kufanya utafiti.
 
Alisema kudumu kwa barabara kutategemea kama masharti yaliyowekwa yatazingatiwa ikiwa ni pamoja na kutopitisha magari makubwa yaliyozidi uzito uliopendekezwa na kwamba atakayebainika kupitisha gari zito atatozwa faini ya shilingi 300,000 na kifungo jela.
 
Aidha katika mkutano huo wanachama wapya wa Chama cha Mapinduzi walikabidhiwa kadi wakiongozwa na mfanyabiashara maarufu katika mji wa Mbalizi, Benson Mwakilembe ambaye awali ilisemekana alikuwa akikifadhili chama cha Demokrasia na maendeleo.
 
Akizungumza baada ya kukabidhiwa kadi, Mwakilembe alisema kwa muda mrefu amekuwa akisaidia shughuli za maendeleo katika mji mdogo wa Mbalizi lakini amekuwa akihusishwa na Chadema jambo ambalo ameamua kuliepuka kwa kuchukua kadi rasmi ya CCM.
 
Alisema hatoacha kukisaidia Chama cha mapinduzi katika harakati za kuwaletea maendeleo wananchi na yupo tayari kutoa magari yake muda wowote itakapohitajika kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.
 
Na Mbeya yetu


No comments: