Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, June 3, 2015

DC MBEYA AWAFUNDA WANAFUNZI

Afisa tawala wa shule za St. Marys Mbeya, Anuciatha Ngonyani akitoa salamu katika sherehe za kutimiza miaka kumi tangu kufunguliwa kwa shule hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Nyerembe Munasa ambaye alikuwa mgeni akitoa hotuba.

Wanafunzi wa St Marys wakiwa kwenye ukumbi wa mikutano.

vijana wa skauti wakionesha uwezo wao wa kupita kwenye kamba


Mkuu wa Wilaya akivalishwa skafu na vijana wa skauti

Wanakwaya wakiwa ukumbini wakifuatilia matukio


                Mkuu wa Wilaya akipewa zawadi
    

MKUU  wa Wilaya ya Mbeya, Nyerembe Munasa ametoa wito kwa wanafunzi nchini kupendelea masomo ya Sayansi kutokana na taifa kwenda kwenye mabadiliko ya sayansi na teknolojia.

Munasa alitoa wito huo  katika sherehe za maadhimisho ya kutimiza miaka kumi kwa Shule ya St. Marys International tangu kuanzishwa kwake Mkoani Mbeya ambapo alikuwa mgeni rasmi.

Alisema Taifa linakoelekea ni kwenye matumizi ya teknolojia mbali mbali hivyo linahitaji wasomi ili waweze kuendana na kasi hiyo hivyo jambo la msingi ni kwa wanafunzi kukazania masomo ya sayansi ili yaweze kuwasaidia baadaye katika kukabiliana na tatizo la ajira.

“Tunataka taifa la wanaosoma sayansi, na karne hii ni sayansi hivyo pendeni masomo ya sayansi, hivi sasa kunamatumizi makubwa ya mitandao ya kijamii pia tumieni hiyo kupata vitu vitakavyowasaidia kimasomo” alisema Mkuu huyo wa Wilaya.

Kwa upande wake Afisa Tawala wa Shule hiyo, Anuciatha Ngonyani, alisema shule hiyo licha ya kupata mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka kumi tangu ianzishwe tawi mkoani Mbeya bado inakabiliwa na changamoto nyingi.

Ngonyani alisema shule hiyo iliyofunguliwa Januari 20, 2005, inakabiliwa na uhaba wa nyumba za walimu, upungufu wa usafiri kwa wanafunzi wa kutwa na kusababisha kukodi magari kwa gharama kubwa, upungufu wa viwanja bya michezo kama mpira wa kikapu na mpira wa mikono.

Aliongeza kuwa bado changamoto kwa Serikali kuzirundikia kodi nyingi shule binafsi pia inapelekea kushindwa kuwalipa Walimu na watumishi wengine mishahara mizuri licha ya kupunguza tatizo la ajira kwa kuwa na watumishi ambao ni walimu na wasio walimu zaidi ya 120.

Alisema Kodi ambazo Serikali inapaswa kuzipunguza katika shule binafsi ni pamoja na Kodi ya ardhi, kodi ya majengo, kodi ya zimamoto na uokoaji, kodi ya Afya za wafanyakazi(OSHA), kodi ya leseni ya biashara, kodi ya uzoaji taka na kodi ya mapato.

                                     Mwisho. 

                                                                           Na Mbeya yetu


No comments: