Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, May 29, 2015

WANANCHI WATEMBEA WABEBA WAGONJWA KWENYE MACHELA WILAYA YA MBEYA

Wananchi wa Kijiji cha Idimi Kata ya Ihango, wilaya ya Mbeya,  wakimbeba mgonjwa kwa kutumia Machela kwenda  Zahanati ya kawatele yenye umbali wa kilometa 10



Mkazi wa kijiji cha Idimi, Rose Sumuni  alisema kina mama wajawazito wamekuwa   wakiteseka hususani wakati wa kujifungua ambapo  wengine wamekuwa wakijifungulia njiani na wengine kupoteza maisha wao wenyewe ama watoto wakiwa tumboni.

Mwenyekiti wa Kjiji cha Idimi,  Langson Paul alikiri wananchi wake kubebwa kwenye machela na  kusafiri mwendo mrefu kufuata huduma ya matibabu huku akibainisha kwamba kuna jengo la zahanati ambalo lilijengwa kwa nguvu za wananchi wenyewe mwaka 2013 na kufikia usawa wa mtambaa wa panya lakini wanashindwa kuendelea kutokana na ukata wa fedha.

Diwani wa Kata ya Ihango Fosta  Mwalingo alipinga wananchi wake kubebwa kwenye machela  lakini alipobanwa zaidi na maswali ya  waandishi wa habari   alishindwa kutetea hoja yake.


Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Marselin Mlelwa akiongea na waandishi wa habari kijijini hapo





Wananchi wa Kijiji cha Idimi Kata ya Ihango, wilaya ya Mbeya,  wanalazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma za matibabu huku wagonjwa wao  kuwabeba kwenye machela kwenda katika zahanati ya Kawetele.


Mwandishi wa habari hizi alishudia wananchi wakijiji hicho wakiwa wamembeba wenzao kwenye machela wakimpeleka katika Zahanati ya Kawetele umbali wa  zaidi ya kilomita 10.



Wakizungumza na Mbeya yetu,  kijijini hapo  wananchi hao walisema licha ya kijiji hicho kuwa makao makuu ya Kata  lakini wamekuwa wakisafiri umbali  wa zaidi ya kilomita 10 kufuata huduma za matibabu kwa miaka mingi jambo ambalo walidai wamewapoteza ndugu zao kwa nyakati tofauti.



Mkazi wa kijiji hicho, Rose Sumuni  alisema kina mama wajawazito wamekuwa   wakiteseka hususani wakati wa kujifungua ambapo  wengine wamekuwa wakijifungulia njiani na wengine kupoteza maisha wao wenyewe ama watoto wakiwa tumboni.



“Binafsi nilimpoteza mtoto wangu akiwa tumboni, kutokana na umbali wa zahanati ama kituo cha afya kuwa mbali, ambapo hadi kufika Hospitali ya rufaa ya Meta na kufanyiwa oparesheni nilikuta mtoto wangu amekufa” alisema mama huyo.



Mkazi mwingine Mashaka  Saagaje,  alisema kutokana na kutokuwa na huduma yoyote ya matibabu  kila kitongoji walitengeneza machela maalum kwa ajili ya kubebea  wagonjwa.



“kwa kweli tunashida kubwa sana, mama zetu wanapoteza maisha kutokana na  miundombinu ya barabara kuwa mbovu na kutembea mwendo mrefu ambapo tukichoka huwa tunamtua popote ili kupumzika halafu tunaanza tena safari hadi zahanati ya Kawetele” alisema Saagaje.



Mwenyekiti wa Kjiji hicho,  Langson Paul alikiri wananchi wake kubebwa kwenye machela na  kusafiri mwendo mrefu kufuata huduma ya matibabu huku akibainisha kwamba kuna jengo la zahanati ambalo lilijengwa kwa nguvu za wananchi wenyewe mwaka 2013 na kufikia usawa wa mtambaa wa panya lakini wanashindwa kuendelea kutokana na ukata wa fedha.



Wakati wananchi wakitoa malalamiko yao na  mwenyekiti wao kukiri hivyo, Diwani wa Kata hiyo  Fosta  Mwalingo alipinga wananchi wake kubebwa kwenye machela  lakini alipobanwa zaidi na maswali ya  waandishi wa habari   alishindwa kutetea hoja yake.



‘Aaa!!! Sio kweli kwamba bado tunabeba wagonjwa kwenye machela kwani hivi sasa tuna usafiri wa bajaji na pikipiki, lakini jitihada zinaendelea kufanyika kuhakikisha tunamaliza zahanati ambayo imejengwa na wananchi wenyewe” alisema diwani huyo.



Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Marselin Mlelwa  alisema katika halmashauri hiyo kuna vijiji vingi ambavyo wananchi wamejenga zahanti hadi kufikia usawa wa renta hivyo kazi yao kubwa ni kumalizia wapofikia wananchi hivyo wanazipa kipaumbele zahanati ambazo zipo mbali zaidi na vituo vya afya ama zahanati jirani.



“Unajua hili ni agizo la Rais kwamba wananchi wajenge hadi usawa fulani halafu serikali inamalizia, na tumeanza kufanya hivyo, lakini hapa tunaangalia zaidi vijiji ambavyo vipo mbali zaidi na hospitali ya rufaa, mkoa au vituo vya afya lakini kwa hapa Idimi sio mbali na hospitali ya rufaa na mkoa” alisema Mlelwa.





  Na Mbeya yetu

No comments: