Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Monday, May 25, 2015

HOT NEWS: DEREVA WA BASI LA TAQWA LILILOJERUHI ABIRIA 15 ALIA NA MMILIKI WAKE.

Dereva akipata Huduma
 Akipata kifungua Kinywa

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida dereva  wa gari la Taqwa lililopata ajali Mei 11 mwaka huu na kujeruhi watu 15 amesema ametelekezwa na tajiri wake akiwa amelazwa katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.
 
 
Akizungumza na waandishi wa habari alikolazwa Dereva huyo David Mtachi, Wadi namba moja katika hospitali ya Rufaa ya Mbeya alisema wakati ajali ikitokea yeye alikuwa amepokewa  Iringa lakini cha ajabu tangu afikishwe Rufaa hakuna alichopata kutoka kwa tajiri wake.
 
 
Alisema dereva aliyempokea gari kutoka Iringa ni Salum Seleman ambaye alipata ajali eneo la Mswisi Wilaya ya Mbarali Mkoani Hapa na kujeruhi abiria 15 akiwemo yeye.
 
 
Alisema tangu kipindi cha ajali tajiri wake hajawahi kutuma hata salamu za pole wala kumtembelea hospitalini anakoendelea na matibabuambapo alitumia muda huo kuwashukuru madaktari wa Hospitali ya Rufaa kwa kumhudumia vizuri.
 
 
 
Gari hiyo mali ya  kampuni ya Taqwa lenye namba za usajili T 791 BZR aina ya Nissan iliyogongana na magari mengine.
 
 
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa Mbeya, Nyigesa Wankyo alithibitisha kutokea kwa ajili hiyo na kuongeza kuwa Gari hilo  lilikuwa likiendeshwa na dereva aitwaye Salumu Selemani (45) mkazi wa Dar es salaam kisha kuligonga gari lenye namba za usajili T 778 CAN Isuzu ftr likiendeshwa na dereva aitwaye Edwin Luyenga (40) na kisha kugonga kwa nyuma gari T 565 CVB likiwa na tela lenye namba T 836 BBC aina ya Man lililokuwa limeharibika na kuegeshwa.
 
 
Kaimu Kamanda alisema ajali hiyo ilitokea majira ya saa mbili usiku katika kijiji cha Kapyo, kata ya Mahongole, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali, Mkoa wa Mbeya katika barabara kuu ya Mbeya/Njombe.
 
 
Aliwataja majeruhi  katika ajali hiyo ni wanaume tisa (09) na wanawake sita (06) walifahamika kwa majina ya Pamat Umuyu (41) Mkongo, Salumu Rashidi (29) mkazi wa Dsm, Juma Rajabu (34) mkazi wa Zanzibar, Anna Misikita (36) Mkongo,  David Mtachi (43) mkazi wa Dsm, Groli Amani (41) mkazi wa Dsm, Kelvin Jordan (39) mkazi wa Dsm,  Waziri Omary (35) mkazi wa Dsm na Mchembe George (35) mkazi wa Mwanza.
 
 
Wengine ni Lika Ilunga (47) mkazi wa Congo, Majariwa Ramadhani (51) mkazi wa Kagera, Adela Mutomba (46) mkazi wa Congo, Mudy Abdallah (43) mkazi Bukoba na Nasoro mkazi wa Tanga, majeruhi mmoja mwanamke ametibiwa na kuruhusiwa na wengine 14 wamelazwa hospitali ya rufaa Mbeya.
 
 
Aliongeza kuwa chanzo cha ajali ni mwendo kasi wa dereva wa basi ambaye amekamatwa ambapo pia ametoa wito kwa madereva kuwa makini wanapotumia vyombo vya moto ikiwa ni pamoja na kufuata sheria,kanuni na alama za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.

 
Na Mbeya yetu

No comments: