Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, April 3, 2015

Wakulima wameshauriwa kulima mazao mchanganyiko ya biashara na chakula Mbeya

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Marselin Mlelwa wakati wa akizungumza na wakulima wa Kijiji cha Idimi Kata ya Ihango wilayani hapa ikiwa ni maadhimisho ya siku ya wakulima.

Mh. Diwani kata ya IhangoFosta Mwalingo akimkaribisha mgeni rasmi aongee na wakulima

Ofisa kilimo wa Shirika la Mtandao wa Kilimo Hifadhi Barani Afrika (ACTN), Nicholaus Johaness, akitoa taarifa fupi kwa mgeni rasmi


wakulima wa Kijiji cha Idimi Kata ya Ihango wilayani Mbeya wakimsikiiza mgeni rasmi  katika maadhimisho ya siku ya wakulima.


Evaristo Joshua Bwana shamba RUCCDIA akijibu  moja ya maswali toka kwa wakulima wa Idimi

Idi Abed bwana shamba toka YARA akitoa somo kwa wakulima
Fadhili Katimba bwana shamba toka SYNGENTA akitoa somo kwa wakulima

Wakulima wakipata somo katika shamba Darasa


Ofisa kilimo wa Shirika la Mtandao wa Kilimo Hifadhi Barani Afrika (ACTN), Nicholaus Johaness, akitoa somo kwa wakulima katika shamba Darasa






  

Mbeya. Wakulima wameshauriwa  kulima mazao mchanganyiko ya biashara  na chakula ili kujiongezea kipato badala ya kuwa na mtazamo wa zao la aina moja la mahindi  au mpunga.

Rai hiyo ilitolewa  juzi na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Marselin Mlelwa wakati wa akizungumza na wakulima wa Kijiji cha Idimi Kata ya Ihango wilayani hapa ikiwa ni maadhimisho ya siku ya wakulima.

Mlelwa alisema ni muda mwafaka kwa wakulima kubadili aina ya mazao wanayolima na kutazama mazao yenye fursa kubwa ya soko tofauti na mahindi, maharage na mpunga.

“Sio lazima mkulima ung’ang’anie mahindi, mpunga au maharage pekee kama zao la biashara wakati hivi sasa kuna mazao mengi kama vile soya, ngano, ufuta na hata mihogo kwani yana soko kubwa na yanahimili pia hali ya hewa” alisema mkurugenzi huyo.

Kwa upande wake, Ofisa kilimo wa Shirika la Mtandao wa Kilimo Hifadhi Barani Afrika (ACTN), Nicholaus Johaness, alisema wakulima wanatakiwa kutumia mbinu ya kilimo cha kubadilisha mazao katika shamba moja ili kuendeleza rutuba katika ardhi  na sio kulima zao la aina moja kila mwaka.

Alisema wakulima wengi  wamekuwa wakilima na kupata mazao finyu kutokana na kulima zao la aina  moja kila mwaka katika  hivyo ardhi kushindwa kuwa na rutuba nzuri.

Kwa upande wa wakulima walisema kilimo hifadhi kimewasaidia wengi na kujiongezea kipato huku wakisisitiza kwamba kufuata maelekezo ya wataalamu wa kilimo (maofisa ugani) inawasaidia kulima kwa kisasa na kujipatia mazao mengi.

Mkulima wa kijiji hicho, Juma  Mwasile alisema ‘miaka ya nyuma tulikuwa tunalima tu bila kufuata mbinu bora kilimo lakini hivi sasa baada ya kuanza kuwatumia maofisa ugani wengi wetu tumekuwa tukipata mazao mengi” alisema Mwasile.

Mwisho. 
Na Mbeya yetu

No comments: