Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, April 24, 2015

WAKAZI WA JIJI LA MBEYA MPO? MUACHE HII TABIA YA KUTUPA TUPA TAKA HOVYO !


WAKAZI wa Jiji la Mbeya wametakiwa kuacha kutupa taka katika mifereji ya maji na kwenye mito jambo linaloweza kusababisha uharibifu wa miundombinu na na magonjwa ya miripuko.
 
Wito huo ulitolewa jana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya, Dk. Samwel Lazaro, alipokuwa akizungumza na Mtandao huu  kuhusiana na kukithiri kwa taka katika mitaa ya Halmashauri hiyo iliyosababishwa na utaratibu mpya wa uzoaji wa taka ulioanzishwa.
 
Dk. Lazaro alilazimika kutoa kauli hiyo kufuatia kuharibika kwa magari ya kuzoa taka ya Halmashauri ya Jiji na kusababisha takataka kukaa muda mrefu mitaani bila kuzolewa ambapo wananchi hulazimika kuvizia mvua zinaponyesha na kasha kutupa taka katika mitaro ya maji na mifereji.
 
Katika utaratibu mpya ulioanzishwa na Halmashauri ya Jiji la Mbeya, Dk. Lazaro alisema udhibiti wa taka umerudishwa mikononi mwa jamii husika ambapo sheria inamtaka kila anayezalisha takataka inakuwa ni mali yake mwenyewe.
 
Hivi sasa Halmashauri ya Jiji la Mbeya limeondoa utaratibu wa wananchi kukusanya takataka na kulunduka katika maghuba na badala yake wanatakiwa kukusanyia majumbani mwao na kasha kusubiri usafiri wa kuzipeleka kwenye dampo.
 
Aidha tangu utaratibu huo uanze wananchi wamekuwa na malalamiko mengi kutokana na magari hayo kushindwa kupita kwa wakati licha ya kulundika taka kwa muda mrefu jambo linaloleta usumbufu kwa watumiaji wa maeneo yanayotumika kukusanyia taka hizo.
 
Akizungumzia malalamiko hayo, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, Dk. Lazaro alisema changamoto kubwa imetokana na kuharibika kwa magari pindi yanapokuwa yanatakiwa kwenda kusomba taka majumbani lakini hivi sasa Jiji liko kwenye mpango wa kuondokana na adha hiyo baada ya TAMISEMI kuridhia Jiji kununua magari mapya ya taka.
 
Alisema hivi sasa Halmashauri ina magari 7 ambayo kati yake magari manne ni ya kupakia kwa mkono na magari mawili yanabeba makontena lakini matarajio ni kuongeza magari mengine 7 ifikapo Mwezi Julai mwaka huu.
 
Aliyataja aina ya magari mapya yanayotarajiwa kuja kupunguza adha ya takataka katika jiji la Mbeya kuwa ni magari matatu ya kupakiwa kwa mkono na magari manne yatakayokuwa yanabeba makontena.
 
Aliongeza kuwa Halmashauri iko kwenye utaratibu wa kuziachia Kata kuunda vikundi kwa ajili ya kukusanya taka katika maeneo yao ambavyo vitajiendesha kupitia ushuru wa taka utakaochangiwa na wananchi wenyewe.
 
Alisema kwa mujibu wa sheria kila Kaya inapaswa kuchangia shilingi 1000 kwa mwezi kwa ajili ya taka lakini Halmashauri imepunguza na kufanya kila nyumba kuchangia shilingi 500 kwa mwezi.
 
Dk. Lazaro aliongeza kuwa Halmashauri haizuu baadhi ya kata kama wanakubaliana kuongeza kiwango cha kuchangia kama wameona shilingi 1000 au 500 haiwatoshi kwa ajili ya kuondoa taka katika maeneo yao.
 

Alizitaja baadhi ya Kata ambazo tayari zimeanza kutekeleza mpango huo kwa kuunda vikundi vya kukusanya taka ambazo ni Kata ya Forest na Kata ya Mwakibete huku utaratibu ni kuendelea kuzihamasisha kata zingine.

No comments: