Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, November 27, 2014

MBEYA YAZINDUA MPANGO WA MAREKEBISHO YA TABIA NA MPANGO WA UTOAJI MSAADA WA SHERIA KWA WATOTO WANAOKINZANA NA SHERIA.

Kamishna Msaidizi Haki za Mtoto na marekebisho ya Tabia nchini, Rubikira Mushi, akizindua Mpango wa Marekebisho ya tabia na mpango wa utoaji msaada wa sheria kwa watoto wanaokinzana na Sheria. uliyofanyika katika ukumbi wa JM Motel iliyopo Forest Jijini Mbeya

Mwakilishi wa UNICEF  katika uzinduzi huo, Mbelwa Gabagumbi, alisema mfumo wa ulinzi na usalama wa mtoto ni wajibu wa Serikali na kila mwananchi hivyo ni vema kuheshimu mkataba wa kimataifa ambao Tanzania iliridhia wa haki za watoto wa mwaka 1989.


Kaimu Mkurugenzi halmashauri ya wilaya Mbeya Getrude Gisema akitoa taarifa fupi wakati wa uzinduzi huo


viongozi mbali mbali ambao ni wadau wa watoto wakiwemo Dawati la jinsia la Polisi, Ustawi wa Jamii, Watendaji wa kata, Msajili wa Mahakama, Chama cha Wanasheria wakiwa makini kumsikiliza mgeni rasmi



Meneja wa KIHUMBE, Samwel Ptolemy, alisema kutakuwa na faida kubwa baada ya kuanza kutekelezwa kwa mpango huo kwa ufadhili wa UNICEF.
 
Msajiri wa Mahakama Rashidi Chaungu Hakimu mkazi Mwandamizi

Mkuu wa Dawati la Jinsia la Polisi Ndimbwelu Mwalukasa

TLS  Rais mstaafu  Francis Sitole

viongozi mbali mbali ambao ni wadau wa watoto wakiwemo Dawati la jinsia la Polisi, Ustawi wa Jamii, Watendaji wa kata, Msajili wa Mahakama, Chama cha Wanasheria na muwakilishi wa Unicef. walishiriki katika uzinduzi huo




Add caption


SHIRIKA la Kikundi cha Huduma Majumbani Mkoa wa Mbeya(KIHUMBE) kwa ufadhili wa Shirika la kuhudumia watoto duniani(UNICEF) limezindua Mpango wa Marekebisho ya tabia na mpango wa utoaji msaada wa sheria kwa watoto wanaokinzana na Sheria.

Uzinduzi huo ulifanywa na Kamishna Msaidizi Haki za Mtoto na marekebisho ya Tabia nchini, Rubikira Mushi, katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa JM Motel iliyopo Forest ya zamani na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali ambao ni wadau wa watoto wakiwemo Dawati la jinsia la Polisi, Ustawi wa Jamii, Watendaji wa kata, Msajili wa Mahakama, Chama cha Wanasheria na muwakilishi wa Unicef.

Akizungumzia Marekebisho ya tabia kwa watoto wanaokinzana na sheria na waliokatika hatari ya kukinzana na sheria, Meneja wa KIHUMBE, Samwel Ptolemy, alisema kutakuwa na faida kubwa baada ya kuanza kutekelezwa kwa mpango huo kwa ufadhili wa UNICEF.

Ptolemy alisema mpango huo utafanikiwa endapo uwepo wa rasilimali watu wa kutekeleza mpango na kutoa mrejesho, kuweka sehemu ambayo watoto watapata mafunzo na elimu kwa kushirikiana na wadau, Ushirikiano baina ya Wadau na Serikali katika kutoa huduma ndani ya jamii.

Aliongeza kuwa faida za mpango huo ni kupunguza idadi ya makosa ya jinai yanayowakumba watoto baada ya kupatiwa elimu, mtoto ataweza kuhudhuria shughuli za maendeleo, kuhudhuria masomo na hatimaye kubadili tabia na kuwa mtoto mwema katika jamii.

Kwa upande wake mwakilishi wa UNICEF  katika uzinduzi huo, Mbelwa Gabagumbi, alisema mfumo wa ulinzi na usalama wa mtoto ni wajibu wa Serikali na kila mwananchi hivyo ni vema kuheshimu mkataba wa kimataifa ambao Tanzania iliridhia wa haki za watoto wa mwaka 1989.

Alisema Tanzania kuna changamoto kubwa ya kufikia malengo kutokana na Halmashauri nyingi kutotenga fedha za kutosha kwa ajili ya maswala ya ulinzi na usalama wa watoto hali inayokwamisha utekelezaji wa mipango mbali mbali inayowekwa na serikali.

Aliongeza kuwa utafiti uliofanywa unaonesha baadhi ya Halmashauri kutenga asilimia 0.002 katika bajeti zao kwa ajili ya siku ya mtoto wa afrika na sio Ulinzi na usalama wa mtroto kama mpango uliozinduliwa unavyotaka.

Akizindua rasmi mpango huo, Kamishna msaidizi Haki za mtoto na marekebisho ya tabia, Rubikira Mushi, mbali na kuyapongeza mashirika ya Kihumbe na Unicef pia aliwapongeza wadau wa watoto Mkoa wa Mbeya kwa kuwa na uelewa wa kuhusu matatizo ya watoto.

Alisema Mpango ulishazinduliwa kwa mara ya Kwanza Mkoani Dar Es Salaam na kufuatiwa na Mkoa wa Mbeya na kuongeza kuwa Sababu zilizopelekea Mkoa wa Mbeya kuwa pili kuzinduliwa kwa mpango huo kuwa ni pamoja na uwepo wa dawati la jinsia la Polisi.

Alizitaja sababu zingine kuwa ni Uwepo wa ofisi za Waendesha mashtaka wa Serikali na Wanasheria wa Serikali,Maafisa ustawi wa jamii wanaoshughulikia mashauri ya watoto, Maafisa ustawi wa jamii hadi ngazi ya kata, timu imara ya ulinzi na usalama wa watoto pamoja na Chama cha Tanganyika Law Society(TLC) kujitolea kutoa msaada bure kuhusiana na maswala ya watoto.

Aliongeza kuwa sababu nyingine ni kuonekana kwa watoto wadogo katika magereza ya wakubwa wakishikiliwa kwa makosa mbali mbali jambo lililopelekea kuzinduliwa kwa mpango huo katika Mkoa wa Mbeya.

Mwisho.

Na Mbeya yetu



No comments: