Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, July 10, 2014

ASKOFU MKUU WA TAG AWAONGOZA WACHUNGAJI KUCHANGIA DAMU


ASKOFU mkuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Dk. Barnabas Mtokambali akichangia Damu

Baadhi ya wachungaji wa kanisa la TAG wakitoa damu na wengine wakisubiri zamu yao


ASKOFU mkuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Dk. Barnabas Mtokambali akipimwa Damu

Makamu Askofu Mkuu, Dk. Mhiche akipimwa damu kabla ya kutoa

Baadhi ya wachungaji wengine wakiwa katika foleni ya kujiandikisha kutoa Damu




ASKOFU mkuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Dk. Barnabas akiongea na waandishi wa habari

Afisa tabibu wa Damu Salama kanda ya Nyanda za juu kusini yenye makao makuu katika Hospitali ya Wazazi Meta jijini Mbeya, Alex Kasimba akiongea na waandishi wa habari


ASKOFU mkuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Dk. Barnabas Mtokambali amewaongoza wachungaji zaidi ya 800 kuchangia damu.

Zoezi hilo liefanyika katika Chuo cha Biblia kilichopo Itende jijini Mbeya ambapo Askofu huyo katika kuonesha uzinduzi na yeye alichangia.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuchangia, alisema Wachungaji wameona wachangie damu kutokana na upungufu na mahitaji yanayoikabili Benki ya damu salama.

Alisema katika zoezi hilo ni wachungaji 800 ambao ni waangalizi wa kanisa ndiyo watakaoanza kuchangia na kufuatiwa na wachungaji wote kutona nchi nzima ambao watakuwepo mkoani Mbeya kwenye maadhimisho ya miaka 75 ya TAG.

Askofu alisema uchangiaji damu huo ni moja ya adhima ya kanisa ili kukabiliana na upungufu wa damu unaokikabili kituo cha damu salama kanda ya Nyanda za juu kusini hivyo litaendeshwa kwa muda wa siku tatu kuanzia Julai 10 hadi 12,mwaka huu ili kukamilisha wachungaji zaidi ya 1000 nchi nzima.

Alisema kama kanisa na Viongozi wameguswa na tatizo la upungufu wa damu katika mahospitali kutokana na watu kupata ajali kila siku, wanawake kupoteza damu nyingi wakati wa kujifungua pamoja na watoto ndiyo maana wakaona ni vema wakaonesha mfano wa kuchangia damu.

Aidha alitoa wito kwa viongozi wengine wa dini bila kujali itikadi zao kuchangia damu popote pale walipo ili kuokoa maisha ya Watanzania wenye mahitaji kwa kuwa damu haiuzwi na hakuna kiwanda cha kuzalisha zaidi ya mtu kujitolea.

Kwa upande wake Afisa tabibu wa Damu Salama kanda ya Nyanda za juu kusini yenye makao makuu katika Hospitali ya Wazazi Meta jijini Mbeya, Alex Kasimba,alisema ni kweli kuna upungufu mkubwa wa damu katika Benki yao.

Alisema kwa takwimu za Mwaka jana damu iliyokuwa ikihitajika ni chupa 28000 lakini Benki ilifanikiwa kukusanya chupa 19000 sawa na asilimia 68 hivyo kuwa na upungufu wa chupa 9000 sawa na asilimia 32.

Alisema hata mwaka huu wanauhitaji wa kiasi kama hicho ili kuweza kuziba pengo la upungufu wa damu ambapo kupitia maadhimisho ya Miaka 75 ya TAG wanatarajia kukusanya zaidi ya Lita 400.

Aliongeza kuwa taasisi za kidini kama TAG, Sabato, Waislam na taasisi za elimu kama Shule za sekondari na vyuo ndiyo wanaojitolea kwa wingi damu tofauti na wananchi wa kawaida.
Mwisho.

 Na Mbeya yetu



No comments: