Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Sunday, April 27, 2014

PSI YATOA MAFUNZO KWA MAWAKALA WA BIDHAA ZA AFYA KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI.


Mgeni rasmi katika Semina hiyo, Dk. Sewangi, ambaye pia ni mratibu wa Ukimwi Mkoa wa Mbeya aliwataka mawakala na wadau mbali mbali kushirikiana na serikali katika kupunguza hali ya maambukizi katika Mikoa ya Kanda ya Kusini.

Mratibu wa shughuli za Operesheni wa PSI Kanda ya Nyanda za Juu kusini, Elia Ndutila, akisoma taarifa fupi wakati wa kufungua mafunzo kwa mawakala wa usambazaji wa bidhaa za afya  iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Paradise Soweto jijini Mbeya.

Baadhi ya mawakala wakimsikiliza mgeni rasmi





Mwezeshaji katika semina hiyo Laurent Mushi akitoa mafunzo kwa mawakala


Picha ya pamoja


MIKOA ya Nyanda za juu kusini imeonekana kuwa bado ni kinara wa magonjwa ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi kitaifa licha ya kuwepo kwa mikakati na kampeni nyingi za kupunguza hali hiyo.

Hayo yamebainishwa na Mratibu wa shughuli za Operesheni wa PSI Kanda ya Nyanda za Juu kusini, Elia Ndutila, wakati wa kufungua mafunzo kwa mawakala wa usambazaji wa bidhaa za afya  iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Paradise Soweto jijini Mbeya.

Ndutila alisema sababu ya kanda hiyo kuongoza kwa maambukizi inatokana na kuwepo kwa shughuli kubwa za kiuchumi pamoja na mashamba makubwa yanayokusanya watu wa aina mbali mbali.

Alisema sababu nyingine ni muingiliano wa watu kutokana na utamaduni wa watu kutoka Mikoa hiyo kufanana pamoja na uwepo wa barabara kuu iendayo nchi jirani hivyo kusababisha wageni wengi kuingia na kutoka kwa shughuli mbali mbali hivyo kuchangia kuwepo kwa maambukizi mapya.

Aidha akizungumzia lengo la Semina hiyo alisema ni kujadili changamoto wanazokabiliana nazo wasambazaji wa bidhaa za PSI katika Mikoa yao ambao wengi wao ni wamiliki wa maduka makubwa ya madawa na mawakala wa bidaa za kawaida.

Alisema mbali na changamoto hizo pia mawakala watajadili malengo ya Mikoa iliyojiwekea kwa ajili ya kuhakikisha inatimiza Sifuri tatu kwa kufikisha kwenye sifuri maambukizi, Vifo na unyanyapaa.

Kwa upande wake Mgeni rasmi katika Semina hiyo, Dk. Sewangi, ambaye pia ni mratibu wa Ukimwi Mkoa wa Mbeya aliwataka mawakala na wadau mbali mbali kushirikiana na serikali katika kupunguza hali ya maambukizi katika Mikoa ya Kanda ya Kusini.

Alisema malengo hayo yanaweza kufikiwa kutokana na serikali kushirikisha Sekta binafsi (PPP) katika kufikia malengo yaliyowekwa ikiwa ni pamoja na kupunguza vifo vya uzazi wa mama na Mtoto.

Mwisho.

Na Mbeya yetu

No comments: