Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, April 8, 2014

MTENDAJI WA KIJIJI AKAMATWA MKUTANONI KWA WIZI WA MIFUKO 189 YA MBOLEA YA RUZUKU

Mtendaji wa Kijiji cha Iwiji Kata ya Iwiji Wilaya ya Mbeya Mkoani Mbeya Anthon Ndisa akielekea kupanda gari ya polisi baada ya kutuhumiwa kuiba mifuko 189 ya mbolea ya ruzuku 


 Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mbeya aliyesimama  Richard Mchovu amesema kuna taratibu za kiutawala zilikiukwa hivyo watafungua jalada la uchunguzi kwa mtendaji wa kijiji hicho na kumpatia mwajiri wake ambaye ni Mkurugenzi wa Wilaya na ikithibitika hatua za kinidhamu zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani.


Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo


Moja kati ya wananchi walipata msukosuko wa kutiwa ndani na mtendaji huyo kwa kisa cha kufuatilia mbolea hiyo






Mtendaji wa Kijiji cha Iwiji Kata ya Iwiji Wilaya ya Mbeya Mkoani Mbeya Anthon Ndisa anashikiliwa na Jeshi la Polisi kuhusiana na upotevu wa Mbolea za ruzuku mifuko 189 kwa kipindi cha mwaka 2013/2014.

Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya Ahmed Msangi amethibitisha kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wa Iwiji na kumtuma Mkuu wa Polisi wilaya ya Mbeya Richard Mchomvu ili kujua hatma ya suala hilo.

Katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijijini hapo na kuhudhuriwa na Afisa tarafa Sote ambapo Afisa Kilimo Maserlin Mlelwa alitoa takwimu za mgao wa mbolea kwa kijiji hicho na utaratibu uliotakiwa kufuatwa kugawa mifuko hiyo 189.

Ndisa alipotakiwa kujieleza katika mkutano huo amedai kuwa alilazimika kuwatumia wenyeviti wa vitongoji kutokana na kamati ya mbolea ya kijiji kuvunjwa na wananchi hao jambo ambalo wananchi walilipinga.

Mbolea hiyo imetolewa na Serikali Mwishonni mwa mwaka jana lakini imedaiwa mbolea hiyo haikuwafikia walengwa na kuleta malalamiko kijijini lawama kubwa ikielekezwa kwa mtendaji wa kijiji Anthon Ndisa aliyepewa dhamana ya kusimamia ugawaji wa pembejeo hizo.

Kwa upande wake Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mbeya Richard Mchovu amesema kuna taratibu za kiutawala zilikiukwa hivyo watafungua jalada la uchunguzi kwa mtendaji wa kijiji hicho na kumpatia mwajiri wake ambaye ni Mkurugenzi wa Wilaya na ikithibitika hatua za kinidhamu zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani.

Mkutano huo pia ulimtupia lawama Diwani wa Kata hiyo Anderson Kabenga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kwa kufumbia macho kero za wananchi licha ya kupewa taarifa mara kwa mara.

Aidha wananchi hao walikerwa na kitendo cha mtendaji kuwakamata wananchi waliokuwa wakifuatilia mgao wa mbolea kwa madai ya kumtishia kuuawa tukio lililofanyika Mwezi Februari mwaka huu na kwenda Polisi Kituo cha Ileje badala ya Mbeya.

Na Ezekiel Kamanga 
Mbeya yetu

No comments: