Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, April 17, 2014

FFU MBEYA YAFANYA MAZOEZI YA KUKABILIANA NA UHALIFU, MKUU WA MKOA WA MBEYA ASHUHUDIA.


MKUU wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro na maafisa wa polisi mkoa wa Mbeya wakiangalia mazoezi ya kikosi cha FFU Mbeya
MKUU wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akiongea na kikosi cha FFU Mbeya


MKUU wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro amelitaka Jeshi la Polisi kujifunza mbinu mbali mbali za kukabiliana na majambazi kutokana na kukithiri kwa vitendo hivyo katika jamii na kuhatarisha usalama wa raia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi alisema utaratibu wa kufanya mazoezi kwa askari wa kupambana na kutuliza ghasia hufanyika mara mbili kwa wiki ikiwa na lengo la kuangalia hali ya nidhamu, ukakamavi na utayari wa Askari katika kupambana na uhalifu.






Mazoezi yakiendelea


Add caption




MKUU wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro amelitaka Jeshi la Polisi kujifunza mbinu mbali mbali za kukabiliana na majambazi kutokana na kukithiri kwa vitendo hivyo katika jamii na kuhatarisha usalama wa raia.

Aidha aliwataka Wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi la Polisi na Vyombo vya ulinzi ili kudumisha amani na utulivu kwa kushiriki kutoa taarifa za uhalifu pamoja na ulinzi shirikishi kwa kutii sheria bila shuruti.

Kandoro alitoa kauli hiyo  alipotembelea mazoezi ya Askari wa Kutuliza ghasia(FFU) mkoani hapa katika viwanja vyao mazoezi yenye lengo la kudumisha nidhamu, ukakamavu na utayari wa kukabiliana na adui kwa Askari wa Jeshi la Polisi.

Alisema jeshi la Polisi pekee haliwezi kudumisha hali ya amani na utulivu kwa Watanzania bila kupata ushirikiano kutoka kwao kwa kutoa taarifa pindi wanapobaini kuwepo kwa hali ya hatari ama uhalifu katika maeneo yao.

Aliongeza kuwa Jeshi la Polisi linatakiwa kuongeza kasi ya kutoa elimu kwa wananchi juu ya utii wa sheria bila shuruti pamoja na ulinzi shirikishi jambo litakalosaidia kupunguza vurugu zisizokuwa na msingi katika jamii.

Alisema pia wananchi hawapaswi kulazimisha Jeshi la Polisi kutumia nguvu kubwa katika kukabiliana nao kutokana na kushindwa kutii amri zinazotolewa na kukatazwa jambo bali watumie njia ya mazungumzo wanapokuwa na madai na siyo kukimbilia kufunga barabara na kuchoma moto.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi alisema utaratibu wa kufanya mazoezi kwa askari wa kupambana na kutuliza ghasia hufanyika mara mbili kwa wiki ikiwa na lengo la kuangalia hali ya nidhamu, ukakamavi na utayari wa Askari katika kupambana na uhalifu.

Katika mazoezi hayo Askari waliweza kumuonesha Mkuu wa Mkoa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Ulinzi na Usalama wa Mkoa mbinu mbali mbali za kukabiliana na maadui ikiwa ni pamoja na kudhibiti vurugu kwa kutumia  mbinu mbali mbali, kukabiliana na majambazi wenye silaha pamoja na mbinu za kivita.

Mwisho.

Na Mbeya yetu



No comments: