Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Monday, March 24, 2014

MAADHIMISHO YA WIKI YA MAJI 2014 JIJI LA MBEYA YAFANA.

 Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji Mbeya, Mhandisi, Simon Shauri, Idrisa Msuya ambaye ni Afisa maji bonde la Ziwa Rufiji na  Mwenyekiti wa bodi wa Mamlaka hiyo, Jaji Atuganile Ngwala wakikata utepe kuzindua mahala pa kunawa mikono kwa wote katika ofisi za mamlaka ya Maji Jijini Mbeya

Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji Mbeya, Mhandisi, Simon Shauri, Idrisa Msuya ambaye ni Afisa maji bonde la Ziwa Rufiji na  Mwenyekiti wa bodi wa Mamlaka hiyo, Jaji Atuganile Ngwala wakiongoza maandamano kuazdhimisha siku ya wiki ya maji 2014 JijiniMbeya







Watoto nao wakishangaa maandamano ya wiki ya maji





Mzee Sefu na Ngoma yake ya kingoni wakitumbuiza kwenye kilele cha maadhimisho ya wiki ya maji





Wimbo wa Taifa ukiimbwa


Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka hiyo, Mhandisi Simioni Shauri  akisoma taarifa mbele ya mgeni rasmi


Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, Idrisa Msuya ambaye ni Afisa maji bonde la Ziwa Rufiji alisema kauli mbiu ya mwaka huu katika kuadhimisha wiki ya maji ni Uhakika wa maji na nishati inatokana na upatikanaji wa nishati ya umeme nafuu kuzalishwa kwa maji.

Mwenyekiti wa bodi wa Mamlaka hiyo, Jaji Atuganile Ngwala akitoa neno la shukrani kwa niaba ya bodi yake ya Maji


MBEYA


ILI kudhibiti na kuhakikisha Mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira Mbeya inakusanya madeni yote kutoka kwa wadaiwa sugu  imeamua kupita nyumba kwa nyumba kwa wateja wenye madeni ili waweze kulipa.

Hatua hiyo imefanyika kwa Mamlaka ya  maji safi na usafi wa Mazingira Mbeya ikishirikiana na Ofisi za Bonde la Ziwa Rukwa, katika kuadhimisha kilele cha wiki ya maji zilizoanza Machi 16, Mwaka huu na kuhitimishwa Machi 22, Mwaka huu kwa mamlaka hiyo kufanya shughuli za usafi.

Akizungumza katika sherehe za maadhimisho hayo zilizofanyika katika viwanja vya Ofisi za Mamlaka ya Maji na usafi wa Mazingira Mbeya, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka hiyo, Mhandisi Simioni Shauri  alisema wiki lote hilo wameshafanya shughuli zaidi ya nne.

Alizitaja shughuli hizo kuwa ni pamoja na usafi kwenye maeneo yote yenye miundombinu ya mamlaka, kutoa elimu kwa wateja kuhusu huduma wanayopewa na kuwahimiza kuilipia kikamilifu ambapo Mamlaka imeamua kupita nyumba kwa nyumba kwa wateja wenye madeni ili waweze kulipa.

Alisema shughuli zingine ni pamoja na kutoa elimu kwa wafanyakazi kuhusu namna miundombinu ya maji safi na majitaka inavyofanya kazi kwa kutembelea miundombinu hiyo pamoja na semina kwa wafanyakazi na wadau kuhusu Huduma bora kwa mteja na umuhimu wa kulipia maji, usimamizi wa vyanzo vya maji na udhibiti wa upotevu wa maji.

Kwa upande wake Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, Idrisa Msuya ambaye ni Afisa maji bonde la Ziwa Rufiji alisema kauli mbiu ya mwaka huu katika kuadhimisha wiki ya maji ni Uhakika wa maji na nishati inatokana na upatikanaji wa nishati ya umeme nafuu kuzalishwa kwa maji.

Alisema maji kwa ajili ya uzalishaji wa nishati ya umeme hayawezi kupatikana iwapo vyanzo vyake havitatunzwa na matumizi yake hayaratibiwa vizuri ili kuondoa matumizi mabaya ya maji pamoja na upotevu.

Alisema uharibifu na matumizi mabaya ya maji yalisababisha kupungua kwa maji katika mabwawa makubwa ya kuzalisha umeme ya Kidatu na Mtera ambayo yalitokana na uharibifu wa vyanzo vya maji katika maeneo ya juu ya mabwawa hayo.

Aliongeza kuwa ni vema kila mtu akishiriki kikamilifu katika kuhakikisha kuwa mipango ya matumizi ya maji yanaratibiwa vyema kisekta ili kuepuka migogoro mikubwa ya watumiaji wenyewe kwa wenyewe na hata kisekta.

Awali maadhimisho hayo yalitanguliwa na maandamano makubwa yaliyowashirikisha wadau wa maji na wafanyakazi wa Mamlaka ya maji na usafi wa mazingira Mbeya pamoja na watumishi wa Bonde la ziwa rukwa.

Na Mbeya yetu

No comments: