Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, March 19, 2014

Ahukumiwa kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kupatikana na hatia ya kunyanyasa na kumtesa mtoto.

MWANAMKE Mwanahawa Nassoro(32) Mkazi wa Mtaa wa Airport jijini Mbeya amehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kupatikana na hatia ya kunyanyasa na kumtesa mtoto.


Baba mzazi wa mtoto John akiwa amekaa na mwanae mara tu baada ya hukumu kutolewa


MWANAMKE Mwanahawa Nassoro(32) Mkazi wa Mtaa wa Airport jijini Mbeya amehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kupatikana na hatia ya kunyanyasa na kumtesa mtoto.

Mwanamke huyo alipandishwa katika Mahakama ya Mwanzo ya Mbeya mjini juzi kutokana na kosa lililokuwa likimkabili la  kumtesa mtoto John Paul(03) ambaye ni mtoto wa kaka yake.

Akisoma mashitaka mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Mbeya mjini, Salome Mwakyosi, mwendesha mashitaka wa Polisi  Kopro Anthon alisema mtuhumiwa alitenda kosa hilo Machi 12, Mwaka huu kwa nyakati tofauti kwa kumfungia ndani na kumnyima chakula kinyume cha sheria namba 241 ya makosa ya jinai sura ya 16 ya kanuni ya adhabu iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Alisema Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Airport, Rehema Mohammed ndiye aliyebaini na kutoa taarifa kwenye uongozi wa Mtaa ambapo mtuhumiwa alikamatwa na hatimaye kufikishwa katika kituo cha Polisi kwa ajili ya hutua za kisheria.

Upande wa Mashitaka ulikuwa na mashahidi wane, ambapo  wawili kati yao ndiyo waliotoa ushahidi ambao ni pamoja na Mjumbe wa Serikali ya Mtaa na Mtoto aliyefanyiwa ukatili huo ambaye alimtambua mahakamani Shangazi yake Mwanahawa licha ya kuwepo watu wengi.

Mtoto huyo alifika mahakamani kutoa ushahidi baada ya afya yake kuimarika kutokana na kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

 Hakimu alipomuuliza mtoto kuhusu mtu aliyekuwa akimpiga alimuonesha Mwanahawa mara tatu ambapo alizidi kumuonesha Shangaza yake huyo.

Kwa upande wake mtuhumiwa wa kesi hiyo alipoulizwa kuhusiana na kosa hilo alikiri ambapo Hakimu aliridhika na ushahidi uliotolewa na pande zote mbili ikiwa ni pamoja na kukiri kwa mtuhumiwa.

Kutokana na ushahidi huo Mahakama hiyo na ilimtia hatiani mshitakiwa kwa kumuadhibu kutumikia  kifungo cha miaka mitatu jela ili iwe fundisho kwa watu wanaofanya vitendo vya kikatili dhidi ya watoto.

Mwisho.

Na Mbeya yetu

No comments: